Kutakaswa Dhambi
1 “Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
2 “Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asemaBwanaMwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
3 Ikiwa yupo ye yote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina laBwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
4 “Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
5 Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
6 Ikiwa mtu atamwuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
Mchungaji Apigwa, Nao Kondoo Watawanyika
7 “Amka, Ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu,
dhidi ya mtu aliye karibu nami!”
asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.
“Mpige mchungaji,
nao kondoo watatawanyika,
nami nitageuza mkono wangu
dhidi ya walio wadogo,
8 katika nchi yote,” asemaBwana,
“theluthi mbili watapigwa na kuangamia;
hata hivyo theluthi moja watabakia ndani yake.
9 Hii theluthi moja nitaileta katika moto;
nitawasafisha kama fedha isafishwavyo
na kuwajaribu kama dhahabu.
Wataliitia Jina langu
nami nitawajibu;
nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’
nao watasema, ‘Bwanani Mungu wetu.’ ”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEC/13-e23899078fb1e45117b740bf03ba066c.mp3?version_id=1627—