1 Mambo ya Nyakati 1

Adamu Hadi Wana Wa Noa

1 Adamu, Sethi, Enoshi,

2 Kenani, Mahalaleli, Yaredi,

3 Henoko, Methusela, Lameki, Noa.

4 Wana wa Noa:

Shemu, Hamu na Yafethi.

Wana Wa Yafethi

5 Wana wa Yafethi walikuwa:

Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.

6 Wana wa Gomeri walikuwa:

Ashkenazi, Rifathi na Togarma.

7 Wana wa Yavani walikuwa:

Elisha, Tarshishi, Kitimu na Warodanimu.

Wana Wa Hamu

8 Wana wa Hamu walikuwa:

# Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.

9 Wana wa Kushi walikuwa:

Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka.

Wana wa Raama walikuwa:

Sheba na Dedani.

10 Kushi alimzaa

Nimrodi aliyekuwa mtu shujaa katika nchi.

11 Misraimu akawazaa

Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi,

12 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti) na Wakaftori.

13 Wana wa Kanaani walikuwa:

Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,

14 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

15 Wahivi, Waariki, Wasini,

16 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi.

Wana Wa Shemu

17 Wana wa Shemu walikuwa:

Elamu, Ashuri, Arfaksadi, Ludi na Aramu.

Wana wa Aramu walikuwa:

Usi, Huli, Getheri na Mesheki.

18 Arfaksadi akamzaa Shela,

Shela akamzaa Eberi.

19 Eberi alikuwa na wana wawili:

# Mmoja wao aliitwa Pelegikwa sababu ni katika wakati wake dunia iligawanyika, ndugu yake aliitwa Yoktani.

20 Wana wa Yoktani walikuwa:

Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

21 Hadoramu, Uzali, Dikla,

22 Obali, Abimaeli, Sheba,

23 Ofiri, Havila na Yobabu. Wote hawa walikuwa wana wa Yoktani.

24 Wana wa Shemu walikuwa Arfaksadi, Shela,

25 Eberi, Pelegi, Reu,

26 Serugi, Nahori, Tera,

27 Tera akamzaa Abramu (yaani, Abrahamu).

Jamaa Ya Abrahamu

28 Abrahamu alikuwa na wana wawili:

Isaki na Ishmaeli.

Wazao Wa Hagari

29 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Hagari:

Nebayothi mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Kedari, Adbeeli, Mibsamu,

30 Mishma Duma, Masa, Hadadi, Tema,

31 Yeturi, Nafishi na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.

Wazao Wa Ketura

32 Wana waliozaliwa na Ketura suria wa Abrahamu walikuwa:

Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua.

Wana wa Yokshani walikuwa:

Sheba na Dedani.

33 Wana wa Midiani walikuwa:

Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa.

Wote hao walikuwa wa uzao wa Ketura.

Wazao Wa Sara

34 Abrahamu alikuwa baba wa Isaki.

Wana wa Isaki walikuwa:

Esau na Israeli.

Wana Wa Esau

35 Wana wa Esau walikuwa:

Elifazi, Rehueli, Yeushi, Yalamu na Kora.

36 Wana wa Elifazi walikuwa:

Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi;

Elifazi kwa Timna akamzaa Amaleki.

37 Wana wa Rehueli walikuwa:

Nahathi, Zera, Shama na Miza.

Watu Wa Seiri Waliokuwa Edomu

38 Wana wa Seiri walikuwa:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani.

39 Wana wa Lotani walikuwa wawili:

Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna.

40 Wana wa Shobali walikuwa:

# Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.

Wana wa Sibeoni walikuwa:

Aya na Ana.

41 Mwana wa Ana alikuwa:

Dishani.

Nao wana wa Dishani walikuwa:

Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

42 Wana wa Eseri walikuwa:

Bilhani, Zaavani na Akani.

Wana wa Dishani walikuwa:

Usi na Arani.

Watawala Wa Edomu

43 Hawa ndio wafalme waliotawala Edomu kabla hajatawala mfalme ye yote wa Waisraeli:

Bela mwana wa Beori, ambaye mji wake ni Dinhaba.

44 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akaingia mahali pake kuwa mfalme.

45 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akaingia mahali pake kuwa mfalme.

46 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akaingia mahali pake kuwa mfalme, mji wake uliitwa Avithi.

47 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akaingia mahali pake kuwa mfalme.

48 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ulio karibu na Mto Eufrati, akaingia mahali pake kuwa mfalme.

49 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akaingia mahali pake kuwa mfalme.

50 Baal-Hanani alipofariki, Hadadi akaingia mahali pake kuwa mfalme. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.

51 Naye Hadadi pia akafa.

Wakuu wa Edomu walikuwa:

Timna, Alva, Yethethi,

52 Oholibama, Ula, Pinoni,

53 Kenazi, Temani, Mibsari,

54 Magdieli na Iramu. Hao ndio wakuu wa makabila ya Edomu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1CH/1-f4c06fda4cc22e1527f752ad96ef473c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine − 6 =