1 Samweli 1

Kuzaliwa Kwa Samweli

1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.

2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.

3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwaBwanaMwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani waBwana.

4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.

5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawaBwanaalikuwa amemfunga tumbo.

6 Kwa sababuBwanaalikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumwudhi.

7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba yaBwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.

8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”

9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu laBwana.

10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwombaBwana.

11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “EeBwanaMwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwaBwanakwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”

12 Alipokuwa anaendelea kumwombaBwana, Eli alichunguza kinywa chake.

13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa

14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo yako.”

15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwaBwana.

16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”

17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”

18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.

19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele zaBwanana kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, nayeBwanaakamkumbuka.

20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwaBwana.”

Hana Anamweka Samweli Wakfu

21 Wakati huyo mtu Elikana alipopanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwaBwanana kutimiza nadhiri yake,

22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele zaBwana, naye ataishi huko wakati wote.”

23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya,Bwanana akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kunyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.

24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya ungana kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba yaBwanahuko Shilo.

25 Wakati walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,

26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwaBwana.

27 Niliomba mtoto huyu, nayeBwanaamenijalia kile nilichomwomba.

28 Hivyo sasa ninamtoa kwaBwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwaBwana.” Naye akamwabuduBwanahuko.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1SA/1-944348c2e6fc8a34714eb69026225c44.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

11 − 11 =