1 Samweli 6

Sanduku La Mungu Larudishwa Israeli

1 Wakati Sanduku laBwanalilipokuwa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba,

2 Wafilisti waliwaita makuhani wa Dagoni na waaguzi na kuwaambia, “Tutafanya nini na hili Sanduku laBwana? Tuambieni jinsi tutakavyolirudisha mahali pake.”

3 Wakajibu, “Kama mtalirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe mikono mitupu bali kwa vyo vyote mpelekeeni sadaka ya hatia. Kisha mtaponywa, nanyi mtafahamu kwa nini mkono wake haujaondolewa kwenu.”

4 Wafilisti wakawauliza, “Ni sadaka gani ya hatia tutakayompelekea?”

Wakajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya wa dhahabu watano, kulingana na idadi ya watawala wa Wafilisti, kwa sababu tauni iyo hiyo imewaua ninyi na watawala wenu.

5 Tengenezeni mifano ya majipu na ya mapanya wale wanaoharibu nchi yenu, nanyi mheshimuni Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka kwenu na kwa miungu yenu na nchi yenu.

6 Kwa nini ninyi mnafanya mioyo yenu migumu kama Wamisri na Farao walivyofanya? Je, alipowatendea kwa ukali, hawakuwaachia Waisraeli wakaenda zao?

7 “Sasa basi, wekeni gari jipya la kukokotwa pamoja na ng’ombe wawili ambao wamezaa lakini ambao kamwe hawajafungwa nira. Fungieni hao ng’ombe hilo gari, lakini ondoeni ndama wao na muwaweke zizini.

8 Chukueni hilo Sanduku laBwanana mliweke juu ya gari la kukokotwa, ndani ya kasha kando yake wekeni hivyo vitu vya dhahabu mnavyompelekeaBwanakama sadaka ya hatia, ipelekeni,

9 lakini liangalieni kwa makini. Iwapo litakwenda katika nchi yake lenyewe, kuelekea Beth-Shemeshi, basi tutajua kwambaBwanandiye aliyeleta haya maafa makubwa juu yetu. Lakini kama halikwenda, basi tutajua kwamba haukuwa mkono waBwanauliotupiga na kwamba iliyotokea kwetu ni ajali.”

10 Basi wakafanya hivyo. Wakachukua ng’ombe wawili wa aina hiyo, wakawafungia hilo gari la kukokotwa, nao ndama wao wakawekwa zizini.

11 Wakaliweka Sanduku laBwanajuu ya hilo gari la kukokotwa pamoja na lile kasha lenye ile mifano ya panya wa dhahabu na ya majipu ya dhahabu.

12 Kisha hao ng’ombe wakaenda moja kwa moja kuelekea Beth-Shemeshi, wakishuka bila kugeuka kuume au kushoto, huku wakilia njia yote. Watawala wa Wafilisti waliwafuata hao ng’ombe hadi mpakani mwa Beth-Shemeshi.

13 Wakati huu watu wa Beth-Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao huko bondeni, walipoinua macho yao na kuona lile Sanduku, wakafurahi kuliona.

14 Lile gari la kukokotwa lilikuja mpaka kwenye shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi, nalo likasimama kando ya mwamba mkubwa. Watu wakapasua mbao za lile gari la kukokotwa na kutoa dhabihu wale ng’ombe kama sadaka ya kuteketezwa kwaBwana.

15 Walawi walilishusha Sanduku laBwana, pamoja na lile kasha lililokuwa na vile vitu vya dhahabu na kuviweka juu ya ule mwamba mkubwa. Siku ile watu wa Beth-Shemeshi wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu kwaBwana.

16 Wale watawala watano wa Wafilisti waliona haya yote, nao wakarudi siku ile ile mpaka Ekroni.

17 Haya ndiyo yale majipu ya dhahabu Wafilisti waliyotuma kama sadaka ya hatia kwaBwana, moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni.

18 Nayo hesabu ya wale panya wa dhahabu ilikuwa kulingana na idadi ya miji ya Wafilisti ya watawala watano wa Wafilisti, na miji yao iliyozungukwa na maboma pamoja na vijiji vya nchi yao. Ule mwamba mkubwa, ambao juu yake waliliweka lile Sanduku laBwana, ni ushahidi hadi leo katika shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi.

19 Lakini Mungu aliwapiga baadhi ya watu wa Beth-Shemeshi, akiwaua watu sabini miongoni mwao kwa sababu walichungulia ndani ya Sanduku laBwana. Watu wakaomboleza kwa sababu ya pigo zito kutoka kwaBwana,

20 nao watu wa Beth-Shemeshi wakauliza, “Ni nani awezaye kusimama mbele zaBwana, huyu Mungu aliye mtakatifu? Sanduku litapanda kwenda kwa nani kutoka hapa?”

21 Kisha wakatuma wajumbe kwa watu wa Kiriath-Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamerudisha Sanduku laBwana. Shukeni na mlipandishe huko kwenu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1SA/6-1dedbf2c43bb98e39b5e3cfeeb80678b.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 × two =