1 Wafalme 14

Unabii Wa Ahiya Dhidi Ya Yeroboamu

1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,

2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.

3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”

4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo.

Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.

5 LakiniBwanaalikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”

6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.

7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyoBwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.

8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.

9 Umefanya maovu mengi kuliko wote walio kutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.

10 “ ‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.

11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.Bwanaamesema!’

12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.

13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambayeBwana, Mungu wa Israeli, ameona walau kitu cho chote chema kwake.

14 “Bwanaatajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.

15 NayeBwanaataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataing’oa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ng’ambo ya Mto Eufrati, kwa sababu wamemghadhibishaBwanakwa kutengeneza nguzo za Ashera.

16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”

17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirza. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.

18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kamaBwanaalivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.

19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha wafalme wa Israeli.

20 Akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme.

Rehoboamu Mfalme Wa Yuda

21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambaoBwanaalikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.

22 Yuda wakatenda maovu machoni paBwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.

23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.

24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayoBwanaaliyafukuza mbele ya Waisraeli.

25 Katika mwaka wa tano wa kutawala kwake Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.

26 Akachukua hazina yote ya Hekalu laBwanana hazina yote ya jumba la kifalme. Alichukua kila kitu, pamoja na ngao zote za dhahabu Solomoni alizotengeneza.

27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba kuweka mahali pa zile za dhahabu, akawagawia wakuu wa ulinzi, waliokuwa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.

28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu laBwana, walinzi walizichukua zile ngao, hatimaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.

29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha wafalme wa Yuda?

30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.

31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiyamwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/1KI/14-6ca50177776e121608a55051c9924c50.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 × five =