2 Mambo ya nyakati 3

Solomoni Ajenga Hekalu

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu laBwanakatika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapoBwanaalikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.

2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa kutawala kwake.

3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitinina upana dhiraa ishirini.

4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini.

Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.

5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.

6 Alilipamba Hekalu kwa mawe ya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.

7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.

8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120za dhahabu safi.

9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.

10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.

11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.

12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.

13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.

14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na za kitani safi na kutarizi makerubi juu yake.

15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.

16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100 na kuyashikamanisha kwenye minyororo.

17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakinina ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2CH/3-afa104b48820ef241793df3f1842922d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fifteen − one =