2 Mambo ya nyakati 32

Senakeribu Aitishia Yerusalemu

1 Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu, mfalme wa Ashuru akaja na kuivamia Yuda. Akaizunguka kwa jeshi miji yenye ngome, akifikiri kuiteka.

2 Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,

3 akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.

4 Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”

5 Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha milokatika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.

6 Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:

7 “Iweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.

8 Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yukoBwanaMungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.

9 Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo kusema:

10 “Hili ndilo Senakeribu Mfalme wa Ashuru asemalo: Je, mmetumainia nini, kwamba mnaendelea kukaa hali mmezungukwa na jeshi katika Yerusalemu?

11 Hezekia asemapo, ‘BwanaMungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, akiwaacha mfe kwa njaa na kiu.

12 Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pakuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Hamna budi kuabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?

13 “Je, hamjui kile mimi na baba zangu tulichokifanya kwa mataifa yote ya nchi nyingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?

14 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza, iliyoweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Ni vipi basi Mungu wenu atakavyoweza kuwaokoa kutoka katika mkono wangu?

15 Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye nakuwapotosha namna hii. Msimwamini kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lo lote wala wa ufalme wo wote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo Mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”

16 Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi yaBwanaaliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.

17 Mfalme pia aliandika barua akimtukanaBwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”

18 Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.

19 Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.

20 Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.

21 NayeBwanaakamtuma malaika ambaye aliangamiza wanaume wote wenye kupigana na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, Mfalme wa Ashuru akarudi kwenye nchi yake mwenyewe kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake walimkata na kumwua kwa upanga.

22 HivyoBwanaakamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote.Bwanaakawastarehesha kila upande.

23 Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili yaBwanana zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.

Kiburi Cha Hezekia, Mafanikio Na Kifo

24 Katika siku zile, Hezekia akaugua naye akawa katika hatari ya kufa. AkamwombaBwanaambaye alimjibu na kumpa ishara.

25 Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu yaBwanaikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.

26 Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu yaBwanahaikuja juu yao katika siku za Hezekia.

27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.

28 Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta, akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.

29 Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ng’ombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

30 Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.

31 Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumwuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.

32 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.

33 Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipokufa. Naye Manase mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2CH/32-fbb162eb4f41bdc35c927fa04448a2b4.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two + 2 =