2 Mambo ya nyakati 33

Manase Mfalme Wa Yuda

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa muda wa miaka hamsini na mitano.

2 Akafanya yaliyo maovu machoni paBwana, akafanya machukizo kama walivyofanya mataifaBwanaaliyoyafukuza mbele ya Waisraeli.

3 Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake, alikuwa amepabomoa, pia akasimamisha madhabahu za Mabaali na nguzo za Maashera. Akalisujudia jeshi lote la vitu vya angani na kuliabudu.

4 Akajenga madhabahu za Baali katika Hekalu laBwanaambamoBwanaalikuwa amesema, “Jina langu litakaa Yerusalemu milele.”

5 Katika nyua zote za Hekalu laBwanaakajengea madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la vitu vya angani.

6 Akawatoa wanawe kuwa kafara kwa kuwapitisha katika moto katika Bonde la Hinomu, akafanya ulozi, uaguzi na uchawi, akataka ushauri kwa wenye pepo wa utambuzi na wenye kuwasiliana na mizimu. Akafanya maovu mengi machoni paBwana, akaichochea hasira yake.

7 Akachukua ile sanamu aliyoichonga akaiweka katika Hekalu laBwanaambalo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele.

8 Sitaifanya miguu ya Waisraeli iondoke tena katika nchi niliyowapa baba zenu, kama watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru kuhusu sheria zote, maagizo na amri zilizotolewa kwa mkono wa Mose.”

9 Lakini Manase akawaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu katika upotovu, kiasi kwamba walifanya maovu mengi kupita mataifa ambayoBwanaaliwaangamiza mbele ya Waisraeli.

10 Bwanaakasema na Manase pamoja na watu wake, lakini hawakumjali.

11 HivyoBwanaakaleta juu yao majemadari wa jeshi la mfalme wa Ashuru, ambao walimchukua Manase kwenda kifungoni, wakaweka ndoana katika pua yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.

12 Katika dhiki yake akamsihiBwanaMungu wake na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.

13 Naye alipomwomba,Bwanaakaguswa na kule kusihi kwake na akasikiliza kilio chake, kwa hiyo akamrudisha Yerusalemu na kwenye ufalme wake. Ndipo Manase akatambua kwambaBwanandiye Mungu.

14 Baadaye akajenga ukuta wa nje wa Mji wa Daudi, magharibi mwa chemchemi ya Gihoni katika bonde, hadi kufikia ingilio la Lango la Samaki na akakizunguka kilima cha Ofeli, pia akaufanya kuwa mrefu zaidi. Akawaweka majemadari katika miji yote ya Yuda iliyokuwa imejengewa ngome.

15 Akaondolea mbali miungu ya kigeni na kuondoa sanamu kutoka katika Hekalu laBwanapamoja na madhabahu zote alizozijenga katika kile kilima kilichojengwa Hekalu na katika Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.

16 Kisha akarudisha madhabahu yaBwanana kutolea juu yake dhabihu za sadaka za amani pamoja na sadaka za shukrani, naye akawaamuru Yuda wamtumikieBwana, Mungu wa Israeli.

17 Lakini hata hivyo watu wakaendelea kutoa dhabihu mahali pa juu pa kuabudia miungu, lakini wakimtoleaBwanaMungu wao peke yake.

18 Matukio mengine ya utawala wa Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno aliyoambiwa na waonaji walionena naye kwa jina laBwana, Mungu wa Israeli, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha wafalme wa Israeli.

19 Maombi yake, pamoja na jinsi Mungu alivyoguswa na kusihi kwake, pia dhambi zake zote na kukosa kwake uaminifu pamoja na sehemu alizojenga mahali pa juu pa kuabudia miungu, kule kusimamisha nguzo za Ashera na sanamu kabla ya kujinyenyekeza kwake, yote yameandikwa katika kumbukumbu za waonaji.

20 Manase akalala pamoja na baba zake akazikwa katika jumba lake la kifalme. Naye Amoni mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme.

Amoni Mfalme Wa Yuda

21 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili, alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili.

22 Akafanya maovu machoni paBwanakama alivyokuwa amefanya Manase baba yake. Amoni akaabudu na kutoa dhabihu kwa sanamu zote alizokuwa ametengeneza Manase.

23 Lakini tofauti na Manase baba yake, hakujinyenyekeza mbele zaBwana, badala yake Amoni aliongeza makosa zaidi na zaidi.

24 Maafisa wa Amoni wakafanya shauri pamoja wakamwua katika jumba lake la kifalme.

25 Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme badala yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2CH/33-9f18842abea748d3ac812d496a7bbd8c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine + nine =