2 Wafalme 16

Ahazi Mfalme Wa Yuda

1 Katika mwaka wa kumi na saba wa kutawala kwake Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.

2 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala kama mfalme, naye akatawala katika Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo sawa mbele ya macho yaBwana, Mungu wake.

3 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli na hata kumtoa mwanawe kafara katika moto, akafuata njia za machukizo za mataifa ambayoBwanaalikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.

4 Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilele vya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.

5 Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.

6 Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi nao wanaishi huko mpaka leo.

7 Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli ambao wananishambulia.”

8 Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu laBwanana katika hazina ya jumba la kifalme na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.

9 Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumwua Resini.

10 Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaiona madhabahu huko Dameski na akamtumia Uria kuhani mchoro wa hiyo madhabahu, pamoja na maelezo yakiwa ya mpango kamili kwa ajili ya ujenzi wake.

11 Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski na kumaliza ujenzi kabla ya kurudi Mfalme Ahazi.

12 Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuiona hiyo madhabahu, aliisogelea na kutoa sadaka juu yake.

13 Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hiyo madhabahu.

14 Mfalme Ahazi akaiondoa ile madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu laBwana, iliyokuwa imesimama kati ya ingilio la Hekalu na hiyo madhabahu mpya, naye akaiweka upande wa kaskazini mwa hiyo madhabahu mpya.

15 Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa kuhani, Uria: “Juu ya hiyo madhabahu kubwa mpya, utoe sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka za kuteketezwa za watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hiyo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hiyo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”

16 Naye Uria, kuhani, akafanya sawasawa kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.

17 Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vinavyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.

18 Kwa ajili ya mfalme wa Ashuru akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu na akafuata ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu laBwana.

19 Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha wafalme wa Yuda?

20 Ahazia akalala pamoja na baba zake naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Hezekia mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2KI/16-e340f60562e2b8a0145fb1aae103b7f1.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × three =