2 Wafalme 3

Moabu Wanaasi

1 Yehoramumwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.

2 Akafanya maovu machoni paBwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.

3 Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.

4 Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo waume 100,000.

5 Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.

6 Kwa hiyo kwa wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya tayari Israeli yote kwenda vitani.

7 Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?”

Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”

8 Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?”

Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”

9 Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba wakitembea, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa pamoja nao.

10 Mfalme wa Israeli akamaka akisema, “Nini! Je,Bwanaametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”

11 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii waBwanahapa, ili tuweze kumwulizaBwanakupitia kwake?”

Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Yeye ndiye aliyekuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”

12 Yehoshafati akasema, “Neno laBwanaliko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.

13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.”

Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu niBwanaambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”

14 Elisha akasema, “Hakika, kamaBwanaMwenye Nguvu Zote aishivyo, ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.

15 Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.”

Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono waBwanaukaja juu ya Elisha,

16 naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyoBwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’

17 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyoBwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ng’ombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.

18 Hili ni jambo rahisi machoni paBwana, ataitia Moabu mikononi mwenu pia.

19 Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”

20 Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.

21 Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao; hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa kwenye mpaka.

22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili, wakaona maji ni mekundu, kama damu.

23 Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima wafalme watakuwa wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”

24 Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.

25 Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake, lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vile vile.

26 Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.

27 Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angeingia mahali pake kuwa mfalme, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2KI/3-dad1484d885c782d9ee3b454cba52592.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eight + 6 =