Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu?
1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu:
2 “Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu,
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3 Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4 Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5 Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6 sembuse mtu ambaye ni funza,
mwanadamu ambaye ni buu tu!”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOB/25-d9dbc23a05f445282c5d246614f53c82.mp3?version_id=1627—