Ayubu 25

Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu?

1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu:

2 “Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu,

yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.

3 Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?

Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?

4 Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?

Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?

5 Ikiwa hata mwezi sio mwangavu

nazo nyota si safi machoni pake,

6 sembuse mtu ambaye ni funza,

mwanadamu ambaye ni buu tu!”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOB/25-d9dbc23a05f445282c5d246614f53c82.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five × 5 =