Danieli 9

Maombi Ya Danieli

1 Katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake Dario mwana wa Ahusuero (mzaliwa wa Umedi) ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,

2 katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, mimi Danieli, nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno laBwanaalilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.

3 Kwa hiyo nikamgeukiaBwanaMungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.

4 NikamwombaBwanaMungu wangu na kutubu:

“Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika Agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,

5 tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi, tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.

6 Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu na watu wote wa nchi.

7 “Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu, wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu nayo Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya sisi kukosa uaminifu kwako.

8 EeBwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.

9 BwanaMungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake,

10 hatukumtiiBwanaMungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.

11 Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii.

“Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.

12 Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka katika Yerusalemu.

13 Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwaBwanaMungu wetu kwa kugeuka kutoka katika dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.

14 Bwanahakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maanaBwanaMungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo, lakini hata hivyo hatujamtii.

15 “Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.

16 Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.

17 “Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako tuangalie kwa huruma kuhusu ukiwa wa mahali pako patakatifu.

18 Ee Mungu, tega sikio na ukasikie, fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.

19 Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”

Majuma Sabini

20 Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli na nikifanya maombi yangu kwaBwanaMungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,

21 wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibia na wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.

22 Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.

23 Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:

24 “Majuma sabini yameamuriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.

25 “Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuweko majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.

26 Baada ya majuma sitini na mawili Mpakwa mafuta atakatiliwa mbali wala hatabakia na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.

27 Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamuriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DAN/9-3b269849c8eb26d361d0f72cb8bb3e9d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five + 11 =