Yerusalemu Mzabibu Usiofaa
1 Neno laBwanalikanijia kusema:
2 “Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wo wote ndani ya msitu?
3 Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza cho chote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuning’inizia vitu kutokana na huo mti wake?
4 Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lo lote?
5 Kama haukufaa kitu cho chote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa cho chote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
6 “Kwa hiyo hili ndiloBwanaMwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
7 Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimiBwana.
8 Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asemaBwanaMwenyezi.”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EZK/15-e257daa6618d40e316467667473c16fb.mp3?version_id=1627—