Ezra 2

Orodha Ya Watu Waliorudi Kutoka Uhamishoni

1 Basi hawa ndio watu wa jimbo, waliotoka uhamishoni ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirejea Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,

2 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana):

Orodha ya watu wa Israeli ilikuwa:

3 wazao wa Paroshi 2,172
4 wa Shefatia 372
5 wa Ara 775
6 wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
7 wa Elamu 1,254
8 wa Zatu 945
9 wa Zaka 760
10 wa Bani 642
11 wa Bebai 623
12 wa Azgadi 1,222
13 wa Adonikamu 666
14 wa Bigwai 2,056
15 wa Adini 454
16 wa Ateri (kwa Hezekia) 98
17 wa Besai 323
18 wa Yora 112
19 wa Hashumu 223
20 wa Gibari 95
21 watu wa Bethlehemu 123
22 wa Netofa 56
23 wa Anathothi 128
24 wa Azmawethi 42
25 wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
26 wa Rama na Geba 621
27 wa Mikmashi 122
28 wa Betheli na Ai 223
29 wa Nebo 52
30 wa Magbishi 156
31 wa Elamu ile ingine 1,254
32 wa Harimu 320
33 wa Lodi, Hadidi na Ono 725
34 wa Yeriko 345
35 wa Senaa 3,630

36 Makuhani:

wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
37 wa Imeri 1,052
38 wa Pashuri 1,247
39 wa Harimu 1,017

40 Walawi:

Wazao wa Yeshua na Kadmieli (wa jamaa ya Hodavia) 74

41 Waimbaji:

Wazao wa Asafu 128

42 Mabawabu wa lango la Hekalu:

Wazao waShalumu, Ateri, Talmoni,Akubu, Hatita na Shobai 139

43 Wanethini:

wazao wa

Siha, Hasufa, tabaothi,

44 Kerosi, Siaha, Padoni,

45 Lebana, Hagaba, Akubu,

46 Hagabu, Shalmai, Hanani,

47 Gideli, Gahari, Reaya,

48 Resini, Nekoda, Gazamu,

49 Uza, Pasea, Besai,

50 Asna, Meunimu, Nefusimu,

51 Bakbuki, Hakufa, Harhuri,

52 Basluthi, Mehida, Harsha,

53 Barkosi, Sisera, Tema,

54 Nesia na Hatifa.

55 Wazao wa watumishi wa Solomoni:

wazao wa

Sotai, Hasaferethi, Peruda,

56 Yaala, Darkoni, Gideli,

57 Shefatia, Hatili,

Pokereth-Hasebaimu na Ami.

58 Wanethini nawazao wa watumishiwa Solomoni 392

59 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuonyesha ya kuwa jamaa zao zilitokana na uzao wa Israeli:

60 Wazao waDelaya, Tobia na Nekoda 652

61 Kutoka miongoni mwa makuhani:

Wazao wa

Hobaya, Hakosi, Barzilai (ambaye alikuwa ameoa binti wa Barzilai Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo.)

62 Hawa walitafuta orodha ya jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kwenye kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.

63 Mtawala aliwaagiza wasile chakula cho chote kitakatifu mpaka awepo kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.

64 Kundi lote lilikuwa na watu 42,360;

65 pamoja na hao kulikuwapo na watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwapo waimbaji wanaume na wanawake 200.

66 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,

67 ngamia 435 na punda 6,720.

68 Walipofika kwenye nyumba yaBwanahuko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika lile eneo lake.

69 Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000za dhahabu, mane 5,000za fedha na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hii.

70 Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na Wanethini waliishi mijini mwao, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi kwenye miji yao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/EZR/2-286d7b4ee7229a577ba3596e7fd918a7.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

10 − 3 =