Hesabu 14

Watu Wanaasi

1 Usiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu.

2 Waisraeli wote wakanung’unika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa!

3 Kwa niniBwanaanatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?”

4 Wakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”

5 Ndipo Mose na Aroni wakaanguka kifudifudi mbele ya kusanyiko lote la Kiisraeli lililokusanyika hapo.

6 Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa watu wale waliokwenda kuipeleleza nchi, wakararua nguo zao,

7 wakasema na kusanyiko lote la Kiisraeli, wakawaambia, “Nchi tuliyopita katikati yake na kuipeleleza ni nzuri sana sana.

8 IkiwaBwanaanapendezwa nasi, atatuongoza kuingia katika nchi ile, nchi itiririkayo maziwa na asali, naye atatupa nchi hiyo.

9 Ila tu msimwasiBwana. Wala msiwaogope watu wa nchi hiyo, kwa sababu tutawameza. Ulinzi wao umeondoka, lakiniBwanayupo pamoja nasi. Msiwaogope.”

10 Lakini kusanyiko lote likazungumza juu ya kuwapiga kwa mawe. Ndipo utukufu waBwanaukaonekana katika Hema la Kukutania kwa Waisraeli wote.

11 Bwanaakamwambia Mose, “Watu hawa watanidharau mpaka lini? Wataendelea kukataa kuniamini mimi mpaka lini, ingawa nimetenda ishara za miujiza miongoni mwao?

12 Nitawapiga kwa tauni na kuwaangamiza, lakini nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa lenye nguvu kuliko wao.”

13 Mose akamwambiaBwana, “Ndipo Wamisri watasikia juu ya jambo hili! Kwa uweza wako uliwapandisha watu hawa kutoka miongoni mwao.

14 Nao watawaambia wenyeji wa nchi hii jambo hili. Wao tayari wameshasikia kwamba wewe, EeBwana, upo pamoja na watu hawa, na kuwa wewe, EeBwana, umeonekana uso kwa uso, nalo wingu lako hukaa juu yao, tena wewe, unawatangulia kwa nguzo ya wingu mchana na kwa nguzo ya moto usiku.

15 Ikiwa utawaua watu hawa wote kwa mara moja, mataifa ambayo yamesikia taarifa hii kukuhusu wewe watasema,

16 ‘Bwanaalishindwa kuwaingiza watu hawa katika nchi aliyowaahidi kwa kiapo; hivyo akawaua jangwani.’

17 “Basi sasa nguvu za Bwana na zionekane, sawasawa na vile ulivyosema,

18 ‘Bwanasi mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo na mwenye kusamehe dhambi na uasi. Lakini haachi kumwadhibu mwenye hatia, huadhibu watoto kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne.’

19 Kwa kadiri ya upendo wako mkuu, usamehe dhambi ya watu hawa, kama vile ulivyowasamehe tangu wakati walipotoka Misri mpaka sasa.”

20 Bwanaakajibu, “Nimewasamehe kama ulivyoomba.

21 Hata hivyo, kwa hakika kama niishivyo, na kwa hakika kama utukufu waBwanauijazavyo dunia yote,

22 hakuna hata mmoja wa watu hawa ambao waliuona utukufu wangu na ishara za miujiza niliyotenda huko Misri na huko jangwani, lakini ambaye hakunitii na akanijaribu mara hizi kumi,

23 hakuna hata mmojawapo atakayeona nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo. Hakuna hata mmoja ambaye amenidharau atakayeiona.

24 Lakini kwa sababu mtumishi wangu Kalebu ana roho ya tofauti na ananifuata kwa moyo wote, nitamwingiza katika nchi aliyoiendea, nao wazao wake watairithi.

25 Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani wanaishi katika mabonde, kesho geukeni mwelekee jangwani kwa kufuata njia iendayo Bahari ya Shamu.”

26 Bwanaakamwambia Mose na Aroni:

27 “Jumuiya hii ovu itanung’unika dhidi yangu hadi lini? Nimesikia malalamiko ya hawa Waisraeli wanaonung’unika.

28 Hivyo waambie, ‘Hakika kama niishivyo, asemaBwana, nitawafanyia vitu vile vile nilivyosikia mkisema:

29 Kila mmoja wenu mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi ambaye alihesabiwa na ambaye amenung’unika dhidi yangu, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.

30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kuwa makao yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.

31 Lakini watoto wenu ambao mlisema watachukuliwa kama mateka, nitawaingiza humo ili waifurahie nchi ambayo ninyi mmeikataa.

32 Lakini ninyi, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.

33 Watoto wenu watakuwa wachungaji wa mifugo hapa kwa miaka arobaini, wakiteseka kwa ajili ya kukosa uaminifu kwenu, hadi mwili wa mtu wenu wa mwisho ulale katika jangwa hili.

34 Kwa miaka arobaini, mwaka mmoja kwa kila siku katika zile siku arobaini mlizoipeleleza nchi, mtateseka kwa ajili ya dhambi zenu, na kujua jinsi ilivyo vibaya kunifanya mimi kuwa adui yenu.’

35 MimiBwananimesema, na hakika nitafanya mambo haya kwa jumuiya hii yote ovu, ambayo imefungamana pamoja dhidi yangu. Watakutana na mwisho wao katika jangwa hili; hapa ndipo watafia.”

36 Hivyo watu wale ambao Mose alikuwa amewatuma kuipeleleza nchi, waliorudi na kuifanya jumuiya nzima kunung’unika dhidi ya Mose kwa kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi,

37 watu hawa waliohusika kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi walipigwa na kuanguka kwa tauni mbele zaBwana.

38 Miongoni mwa watu waliokwenda kuipeleleza hiyo nchi, ni Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune peke yao waliosalia.

39 Mose alipotoa taarifa hii kwa Waisraeli wote, waliomboleza kwa uchungu.

40 Mapema asubuhi siku iliyofuata walipanda juu kuelekea kwenye nchi ya vilima virefu, wakasema, “Tumetenda dhambi. Tutakwea mpaka mahaliBwanaalipotuahidi.”

41 Lakini Mose akasema, “Kwa nini hamtii amri yaBwana? Jambo hili halitafanikiwa!

42 Msipande juu, kwa kuwaBwanahayupo pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu,

43 kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani watapambana nanyi huko. Kwa sababu mmemwachaBwana, hatakuwa pamoja nanyi, ninyi mtaanguka kwa upanga.”

44 Hata hivyo, kwa kiburi chao walipanda juu kuelekea nchi ya vilima virefu, ijapokuwa Mose hakutoka kambini wala Sanduku la Agano laBwana.

45 Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi katika hiyo nchi ya vilima wakatelemka na kuwashambulia, wakawapiga njia yote hadi Horma.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NUM/14-63bb5135a58486d93ccd99ed8ecc6bce.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

thirteen − six =