Hesabu 15

Sadaka Za Nyongeza

1 Bwanaakamwambia Mose,

2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,

3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka katika makundi ya ng’ombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendezaBwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,

4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele zaBwanasadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efaya unga laini uliochanganywa na robo ya hiniya mafuta.

5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.

6 “ ‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efaza unga laini uliochanganywa na theluthi mojaya hini ya mafuta,

7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendezaBwana.

8 “ ‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwaBwana,

9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efauliochanganywa na nusu ya hiniya mafuta.

10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendezaBwana.

11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.

12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.

13 “ ‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendezaBwana.

14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wo wote mgeni au mtu mwingine ye yote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendezaBwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.

15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele zaBwana:

16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’ ”

17 Bwanaakamwambia Mose,

18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka

19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwaBwana.

20 Toeni andazi kutoka katika malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka katika sakafu ya kupuria nafaka.

21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwaBwanakutoka katika malimbuko ya unga wenu.

Sadaka Kwa Ajili Ya Dhambi Isiyo Ya Makusudi

22 “ ‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazoBwanaalimpa Mose,

23 amri yo yote yaBwanakwenu kupitia Mose, tangu siku ileBwanaalipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;

24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendezaBwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.

25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemleteaBwanakwa ajili ya kosa lao sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi.

26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.

27 “ ‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.

28 Kuhani atafanya upatanisho mbele zaBwanakwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, wakati upatanisho utakapokuwa umefanyika kwa ajili yake, atasamehewa.

29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe mzawa ama mgeni.

30 “ ‘Lakini ye yote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuruBwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.

31 Kwa sababu amelidharau neno laBwanana kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima kwa hakika akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’ ”

Mvunja Sabato Auawe

32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.

33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,

34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.

35 NdipoBwanaakamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”

36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kamaBwanaalivyomwamuru Mose.

Vifundo Kwenye Mavazi

37 Bwanaakamwambia Mose,

38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.

39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote zaBwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.

40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.

41 Mimi NdimiBwanaMungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi NdimiBwanaMungu wenu.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NUM/15-0376ac97d713814f2a543c9e91896b18.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

seventeen + fourteen =