Hesabu 17

Kuchipuka Kwa Fimbo Ya Aroni

1 Bwanaakamwambia Mose,

2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.

3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.

4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.

5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manung’uniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”

6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.

7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele zaBwanandani ya Hema la Ushuhuda.

8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.

9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele zaBwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.

10 Bwanaakamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manung’uniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”

11 Mose akafanya sawasawa kamaBwanaalivyomwamuru.

12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!

13 Ye yote akaribiaye Maskani yaBwanaatakufa. Je, sisi sote tutakufa?”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NUM/17-c6ca6c7397bf70c33aa11c7392aaf9de.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

19 − twelve =