Hesabu 18

Wajibu Wa Makuhani Na Walawi

1 Bwanaakamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.

2 Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.

3 Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.

4 Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine ye yote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.

5 “Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.

6 Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwaBwanaili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.

7 Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine ye yote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”

Sadaka Kwa Ajili Ya Makuhani Na Walawi

8 KishaBwanaakamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.

9 Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka katika matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka au za dhambi au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.

10 Myale kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume atayala. Ni lazima myaheshimu kama takatifu.

11 “Hiki pia ni chako: cho chote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kupunga za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.

12 “Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote na divai mpya iliyo bora kuliko zote wanayompaBwanakama malimbuko katika mavuno yao.

13 Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamleteaBwanayatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.

14 “Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwaBwanani chenu.

15 Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwaBwanani wenu. Lakini ni lazima mumkomboe kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.

16 Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tanoza fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.

17 “Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendezaBwana.

18 Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kupungwa na paja la mguu wa kulia.

19 Cho chote kitakachotengwa kutoka katika sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtoleaBwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele zaBwanakwako na watoto wako.”

20 Bwanaakamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wo wote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.

21 “Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.

22 Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.

23 Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wo wote miongoni mwa Waisraeli.

24 Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwaBwanakuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’ ”

25 Bwanaakamwambia Mose,

26 “Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwaBwana, iwe zaka ya hiyo zaka.

27 Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka katika sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.

28 Kwa njia hii ninyi pia mtatoa sadaka kwaBwanakutoka katika zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu yaBwanakwa Aroni, kuhani.

29 Ni lazima mtoe kama sehemu yaBwanailiyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’

30 “Waambie Walawi: ‘Wakati mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.

31 Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali po pote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.

32 Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NUM/18-1d73cb0709c314b39800c9b6fb141162.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

twenty − sixteen =