Hosea 12

1 Efraimu anajilisha upepo;

hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima

na kuzidisha uongo na jeuri.

Anafanya mkataba na Ashuru

na kutuma mafuta ya zeituni Misri.

2 Bwanaanalo shtaka dhidi ya Yuda,

atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake

na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.

3 Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake;

kama mwanadamu, alishindana na Mungu.

4 Alishindana na malaika na kumshinda;

alilia na kuomba upendeleo wake.

Alimkuta huko Betheli

na kuzungumza naye huko:

5 BwanaMungu Mwenye Nguvu Zote,

Bwanandilo jina lake!

6 Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako;

dumisha upendo na haki,

nawe umngojee Mungu wako siku zote.

7 Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu;

hupenda kupunja.

8 Efraimu hujisifu akisema,

“Mimi ni tajiri sana; nimetajirika.

Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu

uovu wo wote au dhambi.”

9 “Mimi ndimiBwanaMungu wenu

niliyewaleta kutoka Misri;

nitawafanya mkae tena kwenye mahema,

kama vile katika siku

za sikukuu zenu zilizoamuriwa.

10 Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi

na kusema mifano kupitia wao.”

11 Je, Gileadi si mwovu?

Watu wake hawafai kitu!

Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali?

Madhabahu zao zitakuwa

kama malundo ya mawe

katika shamba lililolimwa.

12 Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu;

Israeli alitumika ili apate mke,

ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.

13 Bwanaalimtumia nabii

kumpandisha Israeli kutoka Misri,

kwa njia ya nabii alimtunza.

14 Lakini Efraimu amemchochea sana hasira;

Bwana wake ataleta juu yake

hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza

kwa ajili ya dharau yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/12-78dc8f9269267ff93ed97af1852f50f0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

sixteen + 16 =