Hosea 11

Upendo Wa Mungu Kwa Israeli

1 “Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,

nilimwita mwanangu kutoka Misri.

2 Lakini kadiri nilivyomwita Israeli,

ndivyo walivyokwenda mbali nami.

Walitoa dhabihu kwa Mabaali

na kufukiza uvumba kwa vinyago.

3 Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea,

nikiwashika mikono;

lakini hawakutambua

kuwa ni mimi niliyewaponya.

4 Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu,

kwa vifungo vya upendo;

niliondoa nira shingoni mwao

nami nikainama kuwalisha.

5 “Je, hawatarudi Misri,

nayo Ashuru haitawatawala

kwa sababu wamekataa kutubu?

6 Panga zitametameta katika miji yao,

zitaharibu makomeo ya malango yao

na kukomesha mipango yao.

7 Watu wangu wamedhamiria kuniacha.

Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana,

kwa vyo vyote hatawainua.

8 “Efraimu, ninawezaje kukuacha?

Ee Israeli, ninawezaje kukutoa?

Nitawezaje kukutendea kama Adma?

Nitawezaje kukufanya kama Seboimu?

Moyo wangu umegeuka ndani yangu,

huruma zangu zote zimeamshwa.

9 Sitatimiza hasira yangu kali,

wala sitageuka na kumharibu Efraimu.

Kwa kuwa mimi ndimi Mungu,

wala si mwanadamu,

Mtakatifu pekee miongoni mwenu.

Sitakuja kwa ghadhabu.

10 WatamfuataBwana;

atanguruma kama simba.

Wakati angurumapo,

watoto wake watakuja wakitetemeka

kutoka magharibi.

11 Watakuja wakitetemeka

kama ndege wakitoka Misri,

kama hua wakitoka Ashuru.

Nitawakalisha katika nyumba zao,”

asemaBwana.

Dhambi Ya Israeli

12 Efraimu amenizunguka kwa uongo,

nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.

Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu,

hata kinyume cha yeye

aliye mwaminifu Mtakatifu Pekee.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/11-000f60637bc045ab5428ac4196071c11.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

10 − 6 =