Upatanisho Wa Hosea Na Mkewe
1 Bwanaakaniambia, “Nenda, ukaonyeshe upendo wako kwa mke wako tena, ingawa amependwa na mwingine naye ni mzinzi. Mpende kamaBwanaapendavyo Waisraeli, ingawa wanageukia miungu mingine na kupenda mikate mitamu ya zabibu kavu iliyowekwa wakfu.”
2 Basi nilimnunua huyo mwanamke kwa shekeli kumi na tanoza fedha, pia kwa kiasi kama cha homeri moja na nusuya shayiri.
3 Kisha nilimwambia, “Utaishi nami kwa siku nyingi, hupaswi kuwa kahaba au kuwa na uhusiano wa karibu na mtu ye yote, nami nitaishi na wewe.”
4 Kwa maana Waisraeli wataishi siku nyingi bila kuwa na mfalme wala mkuu, bila kuwa na dhabihu wala mawe matakatifu, bila kisibau wala sanamu.
5 Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafutaBwanaMungu wao na Daudi mfalme wao. Watakuja wakitetemeka kwaBwanana kwa baraka zake katika siku za mwisho.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/3-cc76f9180eaa010cd7d5e3abe3bbc37a.mp3?version_id=1627—