Hosea 4

Shtaka Dhidi Ya Israeli

1 Sikieni neno laBwana, enyi Waisraeli,

kwa sababuBwanaanalo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

3 Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu ye yote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

5 Unajikwaa mchana na usiku,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

6 watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

7 Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

8 Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

10 “Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwachaBwana

na kujiingiza wenyewe

11 katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

12 wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

15 “Ingawa umefanya uzinzi, Ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

# usipande kwenda Beth-Aveni.

Wala usiape,

‘Hakika kamaBwanaaishivyo!’

16 Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ng’ombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basiBwanaanaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

17 Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

19 Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/4-23797682a4891b06886ad1291db73701.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

sixteen + one =