Hosea 9

Adhabu Kwa Israeli

1 Usifurahie, Ee Israeli;

usishangilie kama mataifa mengine.

Kwa kuwa hukuwa

mwaminifu kwa Mungu wako;

umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu

ya kupuria nafaka.

2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai

havitalisha watu,

divai mpya itawapungukia.

3 Hawataishi katika nchi yaBwana,

Efraimu atarudi Misri

na atakula chakula

kilicho najisi huko Ashuru.

4 HawatammiminiaBwanasadaka ya divai

wala dhabihu zao hazitampendeza.

Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao

kama mkate wa waombolezaji;

nao wote wailao watakuwa najisi.

Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe;

kisije katika Hekalu laBwana.

5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamuriwa,

katika siku za sikukuu zaBwana?

6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi,

Misri atawakusanya,

# nayo Memfisiitawazika.

Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma,

nayo miiba itafunika mahema yao.

7 Siku za adhabu zinakuja,

siku za malipo zimewadia.

Israeli na afahamu hili.

Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana

na uadui wenu ni mkubwa sana,

nabii anadhaniwa ni mpumbavu,

mtu aliyeongozwa na Mungu

anaonekana mwenda wazimu.

8 Nabii, pamoja na Mungu wangu,

ndiye mlinzi juu ya Efraimu,

hata hivyo mitego inamngojea

katika mapito yake yote,

na uadui katika nyumba ya Mungu wake.

9 Wamezama sana katika rushwa,

kama katika siku za Gibea.

Mungu atakumbuka uovu wao

na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.

10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama

kupata zabibu jangwani;

nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona

matunda ya kwanza katika mtini.

Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu

kwa ile sanamu ya aibu,

nao wakawa najisi

kama kitu kile walichokipenda.

11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege:

hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba,

hakuna kutunga mimba.

12 Hata wakilea watoto,

nitamwua kila mmoja.

Ole wao

nitakapowapiga kisogo!

13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro,

aliyeoteshwa mahali pazuri.

Lakini Efraimu wataleta

watoto wao kwa mchinjaji.”

14 Wape, EeBwana,

je, utawapa nini?

Wape matumbo ya kuharibu mimba

na matiti yaliyokauka.

15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali,

niliwachukia huko.

Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi,

nitawafukuza katika nyumba yangu.

Sitawapenda tena,

viongozi wao wote ni waasi.

16 Efraimu ameharibiwa,

mzizi wao umenyauka,

hawazai tunda.

Hata kama watazaa watoto,

nitawachinja watoto wao

waliotunzwa vizuri.”

17 Mungu wangu atawakataa

kwa sababu hawakumtii;

watakuwa watu wa kutangatanga

miongoni mwa mataifa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/9-cf5284957e19d6f9703ac09c90732ebf.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fourteen − six =