Hosea 10

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana,

alijizalia matunda mwenyewe.

Kadiri matunda yake yalivyoongezeka,

alijenga madhabahu zaidi;

kadiri nchi yake ilivyostawi,

alipamba mawe yake ya ibada.

2 Moyo wao ni mdanganyifu,

nao sasa lazima wachukue hatia yao.

Bwanaatabomoa madhabahu zao

na kuharibu mawe yao ya ibada.

3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme

kwa sababu hatukumheshimuBwana.

Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme,

angeweza kutufanyia nini?”

4 Wanaweka ahadi nyingi,

huapa viapo vya uongo

wanapofanya mapatano;

kwa hiyo mashtaka huchipuka

kama magugu ya sumu

katika shamba lililolimwa.

5 Watu wanaoishi Samaria huogopa

# kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni.

Watu wake wataiombolezea,

vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu,

wale waliokuwa wamefurahia fahari yake,

kwa sababu itaondolewa kutoka kwao

kwenda uhamishoni.

6 Itachukuliwa kwenda Ashuru

kama ushuru kwa mfalme mkuu.

Efraimu atafedheheshwa;

Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.

7 Samaria na mfalme wake wataelea

kama kijiti juu ya uso wa maji.

8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovupataharibiwa:

ndiyo dhambi ya Israeli.

Miiba na mibaruti itaota

na kufunika madhabahu zao.

Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!”

na vilima, “Tuangukieni!”

9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, Ee Israeli,

huko ndiko mlikobaki.

Je, vita havikuwapata

watenda mabaya huko Gibea?

10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu;

mataifa yatakusanywa dhidi yao

ili kuwaweka katika vifungo

kwa ajili ya dhambi zao mbili.

11 Efraimu ni mtamba wa ng’ombe aliyefundishwa

ambaye hupenda kupura,

hivyo nitamfunga nira

juu ya shingo yake nzuri.

Nitamwendesha Efraimu,

Yuda lazima alime,

naye Yakobo lazima avunjevunje

mabonge ya udongo.

12 Jipandieni wenyewe haki,

vuneni matunda ya upendo usio na kikomo,

vunjeni ardhi yenu isiyolimwa;

kwa kuwa ni wakati wa kumtafutaBwana,

mpaka atakapokuja

na kuwanyeshea juu yenu haki.

13 Lakini mmepanda uovu,

mkavuna ubaya,

mmekula tunda la udanganyifu.

Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe

na wingi wa mashujaa wenu,

14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako,

ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa:

kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita,

wakati mama pamoja na watoto wao

walipotupwa kwa nguvu ardhini.

15 Ndivyo itakavyotokea kwako, Ee Betheli,

kwa sababu uovu wako ni mkuu.

Siku ile itakapopambazuka,

mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/HOS/10-8a3954d8315f85488382196086d379dc.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine + 12 =