Isaya 16

Hali Ya Kukata Tamaa Ya Moabu

1 Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi,

Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.

2 Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota chao,

ndivyo walivyo wanawake wa Moabu

kwenye vivuko vya Arnoni.

3 “Tupeni shauri,

toeni uamuzi.

Wakati wa adhuhuri,

fanyeni kivuli chenu kama usiku.

Waficheni watoro,

msisaliti wakimbizi.

4 Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi;

iweni mahali pao pa salama

ili kuepuka mharabu.”

Mtesi atafikia mwisho

na maangamizi yatakoma,

aletaye vita atatoweka kutoka katika nchi.

5 Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa,

kwa uaminifu mtu ataketi juu yake,

yeye atokaye katika nyumba ya Daudi:

yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki,

na huhimiza njia ya haki.

6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu,

kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu,

kiburi chake na ufidhuli wake,

lakini majivuno yake si kitu.

7 Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza,

wanaiombolezea Moabu kwa pamoja.

Wanaomboleza na kuhuzunika

kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

8 Mashamba ya Heshboni yananyauka,

pia na mizabibu ya Sibma.

Watawala wa mataifa

wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana,

ambayo ilipata kufika Yazeri

na kuenea kuelekea jangwani.

Machipukizi yake yalienea

yakafika hadi baharini.

9 Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo,

kwa ajili ya mizabibu ya Sibma.

Ee Heshboni, Ee Eleale,

ninakulowesha kwa machozi!

Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva

na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.

10 Furaha na shangwe zimeondolewa

kutoka katika mashamba ya matunda;

hakuna ye yote aimbaye

wala apazaye sauti

katika mashamba ya mizabibu;

hakuna ye yote akanyagaye zabibu shinikizoni,

kwa kuwa nimekomesha makelele.

11 Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi,

nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.

12 Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu,

anajichosha mwenyewe tu;

anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba,

haitamfaidia lo lote.

13 Hili ndilo neno ambaloBwanaameshasema kuhusu Moabu.

14 Lakini sasaBwanaanasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana tena wanyonge.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/16-d91df6bdb9aa60c24594b248f5d7ef31.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

11 + 19 =