Isaya 15

Unabii Dhidi Ya Moabu

1 Neno kuhusu Moabu:

Ari iliyo katika Moabu imeangamizwa:

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Kiri iliyo katika Moabu imeangamizwa,

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

2 Diboni anakwea hadi kwenye Hekalu lake,

mpaka mahali pake pa juu pa kuabudia miungu ili walie,

Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.

Kila kichwa kimenyolewa

na kila ndevu zimeondolewa.

3 Wamevaa nguo za magunia barabarani,

juu ya mapaa na kwenye viwanja wote

wanaomboleza,

hulala kifudifudi kwa kulia.

4 Heshboni na Eleale wanalia,

sauti zao zinasikika hadi Yahasa.

Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu

wanapiga kelele,

nayo mioyo yao imezimia.

5 Moyo wangu unamlilia Moabu;

wakimbizi wake wanakimbilia Soari,

hadi Eglath-Shelishiya.

Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,

wanakwenda huku wanalia;

kwenye barabara iendayo Horonaimu

wanaombolezea maangamizi yao.

6 Maji ya Nimrimu yamekauka

na majani yamenyauka;

mimea imekauka wala hakuna

kitu cho chote kibichi kilichobaki.

7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba

wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.

8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,

kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,

maombolezo yao hadi Beer-Elimu.

9 Maji ya Dimoni yamejaa damu,

lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:

simba juu ya wakimbizi wa Moabu

na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/15-f1ae431bfd5abb13adc60051601fe9a6.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

11 − 4 =