Isaya 23

Unabii Kuhusu Tiro

1 Neno kuhusu Tiro:

Ombolezeni, Enyi meli za Tarshishi!

Kwa kuwa Tiro imeangamizwa,

imeachwa bila nyumba wala bandari.

# Kuanzia nchi ya Kitimu

neno limewajia.

2 Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani,

pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni,

ambao mabaharia wamewatajirisha.

3 Kwenye maji makuu

nafaka za Shihori zilikuja;

mavuno ya Nile yalikuwa mapato ya Tiro,

naye akawa soko la mataifa.

4 Uaibishwe Ee Sidoni, nawe Ee ngome ya Bahari,

kwa kuwa bahari imesema,

“Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa,

wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”

5 Habari ifikapo Misri,

watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.

6 Vukeni mpaka Tarshishi,

ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.

7 Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe,

mji wa zamani, zamani kabisa

ambao miguu yake imeuchukua

kufanya makao nchi za mbali sana?

8 Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro,

mji utoao mataji,

ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme

na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?

9 BwanaMwenye Nguvu Zote ndiye aliyepanga jambo hili,

ili kukishusha kiburi cha utukufu wote

na kuwanyenyekesha wale wote

ambao ni mashuhuri duniani.

10 Ee Binti Tarshishi,

pita katika nchi yako kama vile Mto Nile

kwa kuwa huna tena bandari.

11 Bwanaamenyosha mkono wake juu ya bahari

na kuzifanya falme zake zitetemeke.

Ametoa amri kuhusu Kanaani

kwamba ngome zake ziangamizwe.

12 Alisema, “Usizidi kufurahi,

Ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa!

“Simama, vuka uende Kitimu;

hata huko hutapata pumziko.”

13 Tazama katika nchi ya Wakaldayo,

watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo!

Waashuri wameifanya nchi hiyo

kuwa mahali pa viumbe wa jangwani.

Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka,

wameziteka ngome zake na kuziacha tupu

na kuufanya kuwa magofu.

14 Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi;

ngome yenu imeangamizwa!

15 Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:

16 “Twaa kinubi, tembea mjini kote,

Ewe kahaba uliyesahauliwa;

piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi,

ili kwamba upate kukumbukwa.”

17 Mwishoni mwa miaka sabini,Bwanaatashughulika na Tiro. Atarudia ajira yake ya ukahaba naye atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.

18 Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa ajili yaBwana; hayatahifadhiwa kwa ajili yake binafsi. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele zaBwanakwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/23-000a34f833cc6a05893a007dcd8cc273.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 + ten =