Isaya 24

Dunia Kuharibiwa Upesi

1 Tazama,Bwanaataifanya dunia kuwa ukiwa

na kuiharibu,

naye atauharibu uso wake

na kutawanya wakaao ndani yake:

2 ndivyo itakavyokuwa

kwa makuhani na kwa watu,

kwa bwana na kwa mtumishi,

kwa bibi na kwa mtumishi wake wa kike,

kwa muuzaji na kwa mnunuzi,

kwa mkopaji na kwa mkopeshaji,

kwa mdaiwa na kwa mdai.

3 Dunia itaharibiwa kabisa

na kutekwa nyara kabisa.

Bwanaamesema neno hili.

4 Dunia inakauka na kunyauka,

dunia inanyong’onyea na kunyauka,

waliotukuzwa wa dunia wananyong’onyea.

5 Dunia imetiwa unajisi na watu wake,

wameacha kutii sheria,

wamevunja amri na kuvunja Agano la milele.

6 Kwa hiyo laana inaiteketeza dunia,

watu wake lazima waichukue hatia yao.

Kwa hiyo wakazi wa dunia wameteketezwa,

nao waliosalia ni wachache sana.

7 Divai mpya inakauka

na mzabibu unanyauka,

watu wote wafurahishao wanalia kwa huzuni.

8 Furaha ya matoazi imekoma,

kelele za wenye furaha zimekoma,

shangwe za kinubi zimenyamaza.

9 Hawanywi tena mvinyo pamoja na wimbo,

kileo ni kichungu kwa wanywaji wake.

10 Mji ulioharibiwa umekuwa ukiwa,

mlango wa kila nyumba umefungwa.

11 Barabarani wanalilia kupata mvinyo,

furaha yote imegeuka kuwa majonzi,

furaha yote imefukuziwa mbali na dunia.

12 Mji umeachwa katika uharibifu,

lango lake limepigwapigwa

na kuvunjwa vipande vipande.

13 Ndivyo itakavyokuwa duniani

na miongoni mwa mataifa,

kama vile wakati mzeituni upigwavyo,

au kama vile wakati masazo yabakiavyo

baada ya zabibu kuvunwa.

14 Wanainua sauti zao, wanapiga kelele kwa furaha,

kutoka magharibi wanasifu kwa ukelele utukufu waBwana.

15 Kwa hiyo upande wa mashariki mpeniBwanautukufu,

liadhimisheni jina laBwana, Mungu wa Israeli,

katika visiwa vya bahari.

16 Kutoka miisho ya dunia tunasikia uimbaji:

“Utukufu kwa yeye Mwenye Haki.”

Lakini nilisema, “Ninadhoofika, ninadhoofika!

Ole wangu!

Watenda hila wanasaliti!

Kwa hila watenda hila wanasaliti!”

17 Hofu, shimo na mtego vinakungojea,

ewe mtu ukaaye duniani.

18 Kila akimbiaye asikiapo sauti ya hofu

atatumbukia shimoni,

ye yote apandaye kutoka shimoni,

atanaswa kwenye mtego.

Malango ya gharika ya mbinguni yamefunguliwa,

misingi ya dunia inatikisika.

19 Dunia imepasuka,

dunia imechanika,

dunia imetikiswa kabisa.

20 Dunia inapepesuka kama mlevi,

inayumbayumba kama kibanda kwenye upepo;

imelemewa sana na mzigo wa hatia ya uasi wake

na ikianguka kamwe haitainuka tena.

21 Katika siku ileBwanaataadhibu nguvu zilizoko mbinguni juu

na wafalme walioko duniani chini.

22 Watakusanywa pamoja

kama wafungwa waliofungwa gerezani,

watafungiwa gerezani

na kujiliwa baada ya siku nyingi.

23 Mwezi utatiwa haya, nalo jua litaaibishwa;

kwa maanaBwanaMwenye Nguvu Zote atawala

juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu,

tena mbele ya wazee wake kwa utukufu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/24-8dc01515934c24aa4e99b6094af8ed27.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

14 + 10 =