Mwaka Wa Upendeleo Wa Bwana
1 Roho waBwanaMwenyezi yu juu yangu,
kwa sababuBwanaamenitia mafuta
kuwahubiri maskini habari njema.
Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo,
kuwatangazia mateka uhuru wao
na hao waliofungwa
habari za kufunguliwa kwao,
2 kutangaza mwaka waBwanauliokubaliwa
na siku ya kisasi ya Mungu wetu,
kuwafariji wote waombolezao,
3 na kuwapa mahitaji
wale wanaohuzunika katika Sayuni,
ili kuwapa taji ya uzuri badala ya majivu,
mafuta ya furaha badala ya maombolezo,
vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa.
Nao wataitwa mialoni ya haki,
pando laBwana
kwa ajili ya kuonyesha utukufu wake.
4 Watajenga upya magofu ya zamani na
kupatengeneza mahali
palipoachwa ukiwa zamani;
watafanya upya miji iliyoharibiwa
iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
5 Wageni watayachunga makundi yenu,
wageni watafanya kazi katika mashamba yenu
na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
6 Nanyi mtaitwa makuhani waBwana,
mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.
Mtakula utajiri wa mataifa,
nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
7 Badala ya aibu yao
watu wangu watapokea sehemu maradufu,
na badala ya fedheha
watafurahia katika urithi wao;
hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao,
nayo furaha ya milele itakuwa yao.
8 “Kwa maana Mimi,Bwana, napenda haki,
ninachukia unyang’anyi na uovu.
Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao
ya haki na kufanya Agano la milele nao.
9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa
na uzao wao miongoni mwa kabila za watu.
Wale wote watakaowaona watatambua
kuwa ni taifa ambaloBwanaamelibariki.”
10 Ninafurahia sana katikaBwana,
nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu.
Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu
na kunipamba kwa joho la haki,
kama vile bwana arusi apambavyo
kichwa chake kama kuhani,
na kama bibi arusi ajipambavyo
kwa vito vyake vya thamani.
11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota
na bustani isababishavyo mbegu kuota,
hivyo hivyoBwanaMwenyezi atafanya haki na sifa
zichipuke mbele ya mataifa yote.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/61-97beb3b5258f8abd70a3e59639a345a3.mp3?version_id=1627—