Isaya 62

Jina Jipya La Sayuni

1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza kimya,

kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,

mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,

wokovu wake kama mwanga wa moto.

2 Mataifa wataona haki yako,

nao wafalme wote wataona utukufu wako;

wewe utaitwa kwa jina jipya

lile ambalo kinywa chaBwanakitatamka.

3 Utakuwa taji ya fahari mkononi mwaBwana,

taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.

4 Hawatakuita tena Aliyeachwa,

wala nchi yako kuiita Ukiwa.

# Bali utaitwa Hefsiba,

# nayo nchi yako itaitwa Beula,

kwa maanaBwanaatakufurahia,

nayo nchi yako itaolewa.

5 Kama vile mwanaume kijana aoavyo mwanamwali,

# ndivyo wanaowatakavyokuoa wewe;

kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,

ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu,

hawatanyamaza mchana wala usiku.

Ninyi wenye kumwitaBwana,

msitulie,

7 msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu

na kuufanya uwe sifa ya dunia.

8 Bwanaameapa kwa mkono wake wa kuume

na kwa mkono wake wenye nguvu:

“Kamwe sitawapa tena adui zenu

nafaka zenu kama chakula chao;

kamwe wageni hawatakunywa tena

divai mpya ambayo hiyo mmeitaabikia,

9 lakini wale waivunao nafaka wataila

na kumsifuBwana,

nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake

katika nyua za patakatifu pangu.”

10 Piteni, piteni katika malango!

Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.

Jengeni, jengeni njia kuu!

Ondoeni mawe.

Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.

11 Bwanaametoa tangazo

mpaka miisho ya dunia:

“Mwambie Binti Sayuni,

‘Tazama, mwokozi wako anakuja!

Tazama ujira wake ukiwa pamoja naye,

na malipo yake yanafuatana naye!’ ”

12 Wataitwa Watu Watakatifu,

Waliokombolewa naBwana;

nawe utaitwa Aliyetafutwa,

Mji Usioachwa Tena.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/62-7cb6a6fcfd003392984c732ae7925927.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 × three =