Isaya 8

Ashuru, Chombo Cha Bwana

1 Bwanaakaniambia, “Chukua gombo kubwa uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida. Maher-Shalal-Hash-Bazi.

2 Nami nitawaita kuhani Uria na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.”

3 Kisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba akazaa mwana. KishaBwanaakaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi.

4 Kabla mtoto hajaweza kusema, ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.”

5 Bwanaakasema nami tena:

6 “Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu

wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,

7 kwa hiyo Bwana yu karibu kuleta dhidi yao

# mafuriko makubwa ya Mto,

mfalme wa Ashuru na fahari yake yote.

Yatafurika juu ya mifereji yake yote,

yatamwagikia juu ya kingo zake zote

8 na kufika hadi Yuda, ukizunguka kwa kasi juu yake,

yakipita kutoka upande huu

mpaka upande mwingine yakifika hadi shingoni.

Mabawa yake yaliyokunjuliwa

yatafunika upana wa nchi yako,

# Ee Imanueli!”

9 Inueni kilio cha vita, enyi mataifa

na mkavunjwevunjwe!

Sikilizeni, enyi nyote nchi za mbali.

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

10 Wekeni mikakati yenu, lakini itashindwa;

fanyeni mipango yenu, lakini haitafanikiwa,

# kwa maana Mungu yu pamoja nasi.

Mwogope Mungu

11 Bwanaalisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:

12 “Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina,

usiogope kile wanachokiogopa,

wala usikihofu.

13 BwanaMwenye Nguvu Zote ndiye peke yake

ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu,

ndiye peke yake utakayemwogopa,

ndiye peke yake utakayemhofu,

14 naye atakuwa mahali patakatifu;

lakini kwa nyumba zote mbili za Israeli atakuwa

jiwe lile linalosababisha watu kujikwaa

na mwamba wa kuwaangusha.

Kwa watu wa Yerusalemu atakuwa

mtego na tanzi.

15 Wengi wao watajikwaa;

wataanguka na kuvunjika,

watategwa na kunaswa.”

16 Funga ushuhuda na

kutia muhuri sheria

miongoni mwa wanafunzi wangu.

17 NitamngojeaBwana,

ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake.

Nitaliweka tumaini langu kwake.

18 Nipo hapa pamoja na watoto ambaoBwanaamenipa. Sisi ni ishara na mfano wake katika Israeli, kutoka kwaBwanaMwenye Nguvu Zote, anayeishi juu ya Mlima Sayuni.

19 Wakati watu wanapowaambia ninyi kutafuta ushauri kwa waaguzi na wenye kuongea na mizimu, ambao hunong’ona na kunung’unika, je, watu wasingeuliza kwa Mungu wao? Kwa nini watake shauri kwa wafu kwa ajili ya walio hai?

20 Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawatasema sawasawa na neno hili, hawana mwanga wa mapambazuko.

21 Wakiwa na dhiki na njaa, watazunguka katika nchi yote, watakapotaabika kwa njaa, watapatwa na hasira kali, wakiwa wanatazama juu, watamlaani mfalme wao na Mungu wao.

22 Kisha wataangalia duniani na kuona dhiki na giza, hofu na huzuni tupu, nao watasukumiwa kwenye giza nene kabisa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/8-6787976f18db72f78a8c589a8c126486.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × five =