Kumbukumbu La Torati 1

Amri Ya Kuondoka Mlima Horebu

1 Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko katika Araba, inayokabiliana na Sufu kati ya Parani na Tofeli, Labani, Hazerothi na Dizahabu.

2 (Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)

3 Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yoteBwanaaliyomwamuru kuwahusu.

4 Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.

5 Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:

6 BwanaMungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.

7 Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea katika nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Eufrati.

8 Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayoBwanaaliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”

Uteuzi Wa Viongozi

9 Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.

10 BwanaMungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.

11 NayeBwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!

12 Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?

13 Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka katika kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”

14 Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”

15 Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.

16 Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.

17 Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu ye yote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lo lote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.

18 Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.

Wapelelezi Wanatumwa

19 Kisha, kamaBwanaMungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.

20 Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayoBwanaMungu wetu anatupa.

21 Tazama,BwanaMungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kamaBwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”

22 Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”

23 Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.

24 Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.

25 Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayoBwanaMungu wetu anatupa.”

Uasi Dhidi Ya Bwana

26 Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri yaBwanaMungu wenu.

27 Mkanung’unika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwanaanatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.

28 Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’ ”

29 Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.

30 BwanaMungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,

31 na pia huko jangwani. Huko mliona jinsiBwanaMungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”

32 Pamoja na hili, hamkumtegemeaBwanaMungu wenu,

33 ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.

34 WakatiBwanaaliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:

35 “Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,

36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuataBwanakwa moyo wote.”

37 Kwa sababu yenuBwanapia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.

38 Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataiingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.

39 Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.

40 Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”

41 Ndipo mkanijibu, “TumemtendaBwanadhambi. Tutakwenda kupigana, kamaBwanaMungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.

42 LakiniBwanaaliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’ ”

43 Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri yaBwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.

44 Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.

45 Mlirudi na kulia mbele zaBwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.

46 Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/1-95cf3f132e5a72c718bff1cef53be6f6.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

11 − 6 =