Yoshua 24

Agano Lafanywa Upya Huko Shekemu

1 Ndipo Yoshua akaita pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na maafisa wa Israeli, nao wakaja mbele za Mungu.

2 Yoshua akawaambia watu wote, “Hili ndiloBwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Hapo zamani baba zenu, pamoja na Tera baba yake Abrahamu na Nahori, waliishi ng’ambo ya Mto Eufrati nao waliiabudu miungu mingine.

3 Lakini nilimwondoa baba yenu Abrahamu kutoka nchi hiyo ng’ambo ya Mto, nami nikamwongoza katika nchi yote ya Kanaani, nikampa wazao wengi. Nikampa Isaki,

4 naye Isaki nikampa Yakobo na Esau. Esau nikampa nchi ya vilima ya Seiri, lakini Yakobo pamoja na wanawe wakashuka Misri.

5 “ ‘Kisha nikawatuma Mose na Aroni, nami nikawapiga Wamisri kwa kile nilichokitenda huko, tena nikawatoa huko.

6 Nilipowatoa baba zenu katika nchi ya Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka kwenye Bahari ya Shamu.

7 Lakini wakamliliaBwanawakitaka msaada, Mungu akaweka giza kati yenu na Wamisri, akaileta bahari juu yao ikawafunika. Ninyi mliona kwa macho yenu wenyewe kile nilichowatendea Wamisri. Kisha mliishi jangwani kwa muda mrefu.

8 “ ‘Nikawaleta katika nchi ya Waamori ambao waliishi mashariki ya Yordani. Wakapigana nanyi, lakini nikawatia mikononi mwenu. Nikawaangamiza mbele yenu nanyi mkaimiliki nchi yao.

9 Wakati Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alipojiandaa kupigana dhidi ya Israeli, alimwita Balaamu mwana wa Beori apate kuwalaani.

10 Lakini sikumkubali Balaamu, kwa hiyo aliwabariki tena na tena, nami niliwaokoa toka mkononi mwake.

11 “ ‘Ndipo mlipovuka Yordani mkafika Yeriko. Raia wa Yeriko wakapigana nanyi, kama walivyofanya Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi, lakini niliwatia mikononi mwenu.

12 Nikatuma manyigu mbele yenu, ambao pia waliwafukuza mbele yenu, hao wafalme wawili wa Waamori. Siyo upanga au upinde wenu wenyewe vilivyowapatia ushindi.

13 Hivyo nikawapa ninyi nchi ambayo hamkuitaabikia na miji ambayo hamkuijenga, mkaishi ndani yake na kula mizabibu na mizeituni msiyoipanda.’

14 “Sasa basi mcheniBwanana kumtumikia kwa uaminifu wote. Itupeni mbali miungu ambayo baba zenu waliiabudu huko ng’ambo ya Mto Eufrati na huko Misri, nanyi mtumikieniBwana.

15 Lakini msipoona vyema kumtumikiaBwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia, kama ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo Eufrati, au miungu ya Waamori, ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikiaBwana.”

16 Ndipo hao watu wakajibu, “Hili liwe mbali nasi la kumsahauBwanana kuitumikia miungu mingine!

17 Ilikuwa niBwanaMungu wetu mwenyewe aliyetutoa sisi na baba zetu akatupandisha kutoka Misri, kutoka nchi ile ya utumwa, na kutenda zile ishara kubwa mbele ya macho yetu. Ndiye aliyetulinda katika safari yetu yote na kutokana na mataifa yote ambayo tulipita katikati yao.

18 Bwanaakawafukuza mbele yetu mataifa yote pamoja na Waamori, walioishi katika nchi hii. Hivyo sisi nasi tutamtumikiaBwana, kwa kuwa yeye ndiye Mungu wetu.”

19 Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikiaBwana. Yeye ni Mungu Mtakatifu, ni Mungu mwenye wivu. Hatasamehe uasi wenu na dhambi zenu.

20 Ikiwa mkimwachaBwanana kuitumikia miungu migeni, yeye atageuka na kuwaleteeni maafa na kuwaangamiza, baada ya kuwa mwema kwenu.”

21 Lakini watu wakamwambia Yoshua, “Sivyo! Sisi tutamtumikiaBwana.”

22 Ndipo Yoshua akawaambia, “Ninyi mmekuwa mashahidi juu yenu wenyewe kuwa mmechagua kumtumikiaBwana.”

Nao wakajibu, “Ndiyo, tu mashahidi.”

23 Yoshua akawaambia, “Sasa basi, itupeni mbali hiyo miungu migeni iliyo katikati yenu, nanyi mtoleeniBwana, Mungu wa Israeli, mioyo yenu.”

24 Nao watu wakamwambia Yoshua, “TutamtumikiaBwanaMungu wetu na kumtii yeye.”

25 Siku ile Yoshua akafanya agano kwa ajili ya watu na hapo Shekemu ndipo alipowaandikia amri na sheria.

26 Naye Yoshua akayaandika mambo haya katika Kitabu cha Sheria ya Mungu. Ndipo akalitwaa jiwe kubwa akalisimamisha huko, chini ya mwaloni huko karibu na mahali patakatifu paBwana.

27 Akawaambia watu wote, “Angalieni! Jiwe hili litakuwa shahidi juu yetu. Limesikia maneno yoteBwanaaliyotuambia. Litakuwa shahidi juu yenu kama mtakuwa waongo kwa Mungu wenu.”

Kuzikwa Katika Nchi Ya Ahadi

28 Basi Yoshua akawatuma watu kila mmoja aende katika urithi wake mwenyewe.

29 Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi waBwanaakafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi.

30 Nao wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Serakatika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima wa Gashi.

31 Israeli wakamtumikiaBwanawakati wote wa kipindi cha Yoshua, na kipindi cha hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa na ambao waliona wenyewe kila kituBwanaalichowatendea Israeli.

32 Nayo ile mifupa ya Yosefu, ambayo Waisraeli waliipandisha kutoka huko Misri, wakaizika huko Shekemu kwenye eneo, ambalo Yakobo alilinunua kwa wana wa Hamori baba yake Shekemu, kwa vipande mia vya fedha. Eneo hili likawa ni urithi wa uzao wa Yosefu.

33 Naye Eleazari mwana wa Aroni akafariki akazikwa huko Gibeathi, ambapo alikuwa amepewa mtoto wake Finehasi, kwenye nchi ya vilima ya Efraimu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOS/24-60870f2732749295a19fb15578d5f092.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

ten − 7 =