Kumbukumbu La Torati 6

Mpende Bwana Mungu Wako

1 Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazoBwanaMungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki,

2 ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamcheBwanaMungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu.

3 Sikia, Ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kamaBwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.

4 Sikia, Ee Israeli:BwanaMungu wako, niBwanammoja.

5 MpendeBwanaMungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote na kwa nguvu zako zote.

6 Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.

7 Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.

8 Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.

9 Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.

10 WakatiBwanaMungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga,

11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,

12 jihadhari usije ukamwachaBwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nchi ya utumwa.

13 UtamchaBwanaMungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.

14 Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;

15 kwa kuwaBwanaMungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka katika uso wa nchi.

16 UsimjaribuBwanaMungu wako kama ulivyofanya huko Masa.

17 Utayashika maagizo yaBwanaMungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.

18 Fanya lililo haki na jema mbele zaBwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayoBwanaaliahidi kwa kiapo kwa baba zako,

19 kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kamaBwanaalivyosema.

20 Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazoBwanaMungu wako alikuagiza wewe?”

21 Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakiniBwanaalitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu.

22 Bwanaakapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote.

23 Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo.

24 Bwanaakatuagiza tutii amri hizi zote na kumchaBwanaMungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo.

25 Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele zaBwanaMungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/6-bc5311edec2b518759d98228f23fe746.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 + 18 =