Kumbukumbu La Torati 7

Kuyafukuza Mataifa

1 BwanaMungu wako akuletapo katika nchi unayoiingia ili kuimiliki na awafukuzapo mbele yako mataifa mengi, yaani, Wahiti, Wagirgashi, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, mataifa saba makubwa tena yenye nguvu kuliko wewe,

2 piaBwanaMungu wako atakapowatia mkononi mwako na ukawashinda, basi ni lazima uwaangamize wote kabisa. Usifanye agano nao, usiwahurumie.

3 Usioane nao. Usimtoe binti yako kuolewa na mwanawe, au kumchukua binti yake aolewe na mwanao.

4 Kwa maana watamgeuza mwanao aache kunifuata, ili aitumikia miungu mingine, nayo hasira yaBwanaitawaka dhidi yako, naye atakuangamiza ghafula.

5 Hili ndilo utakalowafanyia: Vunja madhabahu zao, yabomoe mawe yao yaliyowekwa wakfu, katakata nguzo zao za Ashera na kuchoma sanamu zao kwa moto.

6 Kwa kuwa wewe ni taifa takatifu kwaBwanaMungu wako.BwanaMungu wako amekuchagua wewe kutoka katika mataifa yote juu ya uso wa dunia kuwa watu wake, hazina yake ya thamani.

7 Bwanahakuweka upendo wake juu yenu na kuwachagua kwa sababu mlikuwa wengi mno kuliko watu wengine, kwa maana ninyi ndio mliokuwa wachache sana kuliko mataifa yote.

8 Lakini ni kwa sababuBwanaaliwapenda ninyi na kutunza kiapo alichowaapia babu zenu kwamba atawatoa ninyi kwa mkono wenye nguvu na kuwakomboa kutoka nchi ya utumwa, kutoka nguvu za Farao mfalme wa Misri.

9 Basi ujue kwambaBwanaMungu wako ndiye Mungu; ni Mungu mwaminifu, anayetunza Agano la upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanaompenda na kuzishika amri zake.

10 Lakini

kwa wale wanaomchukia

atawalipiza kwenye nyuso zao

kwa maangamizi;

hatachelewa kuwalipiza kwenye nyuso zao

wale wamchukiao.

11 Kwa hiyo, iweni waangalifu kufuata maagizo, amri na sheria ninazowapa leo.

12 Kama mkizingatia sheria hizi na kuzifuata kwa uangalifu, basiBwanaMungu wenu atatunza Agano lake la upendo nanyi, kama alivyowaapia baba zenu.

13 Atawapenda ninyi na kuwabariki na kuongeza idadi yenu. Atabariki uzao wa tumbo lenu, mazao ya nchi yenu, nafaka, divai mpya na mafuta, ndama wa ng’ombe wa kundi lenu na kondoo za kundi lenu katika nchi ile aliyoapa kuwapa baba zenu.

14 Mtabarikiwa kuliko mataifa mengine yote, hakuna wanaume wala wanawake kwenu watakaokosa watoto, wala mifugo yenu haitakuwa tasa.

15 Bwanaatawakinga na kila ugonjwa. Mungu hatatia juu yenu ugonjwa wo wote mbaya mlioufahamu huko Misri, lakini atatia ugonjwa juu ya wale wote wanaokuchukia.

16 Ni lazima mwangamize watu wote ambaoBwanaMungu wenu atawatia mikononi mwenu. Msiwatazame kwa kuwahurumia na msitumikie miungu yao, kwa kuwa itakuwa mtego kwenu.

17 Mnaweza kujiuliza wenyewe “Mataifa haya ni yenye nguvu kuliko sisi. Tutawezaje kuwafukuza?”

18 Lakini msiwaogope. Kumbukeni vyema jinsiBwanaMungu wenu alivyofanya kwa Farao na kwa wote huko Misri.

19 Mliona kwa macho yenu wenyewe majaribu makubwa, ishara za miujiza na maajabu, mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, ambao kwa huoBwanaMungu wenu aliwatoa mtoke Misri.BwanaMungu wenu atawafanyia hivyo watu wote ambao mnawaogopa sasa.

20 Zaidi ya hayo,BwanaMungu wenu atatuma manyigu miongoni mwao hadi yale mabaki watakaojificha waangamie.

21 Msiingiwe na hofu kwa sababu yao, kwa kuwaBwanaMungu wenu, ambaye yupo miongoni mwenu ni mkuu naye ni Mungu wa kutisha.

22 BwanaMungu wenu atawafukuza mataifa hayo mbele yenu kidogo kidogo. Hamtaruhusiwa kuwaondoa wote kwa mara moja, la sivyo wanyama mwitu wataongezeka na kuwa karibu nanyi.

23 LakiniBwanaMungu wenu atawatia watu hao mikononi mwenu, akiwatia katika kuchanganyikiwa kukubwa mpaka wawe wameangamizwa.

24 Atawatia wafalme wao mikononi mwenu, nanyi mtayafuta majina yao chini ya mbingu. Hakuna hata mmoja atakayeweza kusimama dhidi yenu bali mtawaangamiza.

25 Vinyago vya miungu yao mtavichoma moto. Msitamani fedha wala dhahabu iliyo juu yao, wala msizichukue kwa ajili yenu, la sivyo mtakuwa mmetekwa navyo. Kwa kuwa ni chukizo kwaBwanaMungu wenu.

26 Msilete vitu vya machukizo katika nyumba zenu kwani ninyi, mtatengwa kama vitu hivyo kwa maangamizo. Ukichukie kabisa kitu hicho kwa kuwa kimetengwa kwa maangamizo.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/7-fadc45cb5701ff3fb9ac1fe8a4a350b9.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

four × 4 =