Mika 3

Viongozi Na Manabii Wakemewa

1 Kisha nikasema,

“Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli.

Je, hampaswi kujua hukumu,

2 ninyi mnaochukia mema

na kupenda maovu;

ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi

na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;

3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu,

mnaowachuna ngozi

na kuvunja mifupa yao vipande vipande;

mnaowakatakata kama nyama

ya kuwekwa kwenye sufuria

na kama nyama

ya kuwekwa kwenye chungu?”

4 Kisha watamliliaBwana,

lakini hatawajibu.

Wakati huo atawaficha uso wake

kwa sababu ya uovu waliotenda.

5 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu,

mtu akiwalisha,

wanatangaza ‘amani’;

kama hakufanya hivyo,

wanaandaa kupigana vita dhidi yake.

6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono,

na giza, msiweze kubashiri.

Jua litawachwea manabii hao,

nao mchana utakuwa giza kwao.

7 Waonaji wataaibika

na waaguzi watafedheheka.

Wote watafunika nyuso zao

kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”

8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu,

nimejazwa Roho waBwana,

haki na uweza,

kumtangazia Yakobo kosa lake,

na Israeli dhambi yake.

9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli,

mnaodharau haki

na kupotosha kila lililo sawa;

10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu

na Yerusalemu kwa uovu.

11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa,

na makuhani wake wanafundisha kwa malipo,

nao manabii wake wanatabiri kwa fedha.

Hata hivyo wanamwegemeaBwanana kusema,

“Je,Bwanasi yumo miongoni mwetu?

Hakuna maafa yatakayotupata.”

12 Kwa hiyo kwa sababu yenu,

Sayuni italimwa kama shamba,

Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto

na kilima cha Hekalu

kuwa kama kichuguu

kilichofunikwa na vichaka.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/MIC/3-ab13fe7fa79e1ebce9ede403a655dfa0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 × 4 =