Mithali 18

1 Mtu ajitengaye na wengine

hufuata matakwa yake mwenyewe;

hupiga vita kila shauri jema.

2 Mpumbavu hafurahii ufahamu,

bali hufurahia kutangaza

maoni yake mwenyewe.

3 Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia,

pamoja na aibu huja lawama.

4 Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji,

bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.

5 Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu,

au kumnyima asiye na hatia haki.

6 Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi

na kinywa chake hualika kipigo.

7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake

na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.

8 Maneno ya uchongezi ni kama vyakula vitamu,

huingia sehemu za ndani sana za mtu.

9 Mtu aliye mlegevu katika kazi yake

ni ndugu na yule anayeharibu.

10 Jina laBwanani ngome imara,

wenye haki huikimbilia na kuwa salama.

11 Mali ya matajiri ni mji wao wa ngome,

wanaudhania kuwa ni ukuta usioweza kurukwa.

12 Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi,

bali unyenyekevu hutangulia heshima.

13 Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza,

huo ni upumbavu wake na aibu yake.

14 Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa

bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?

15 Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa,

masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.

16 Zawadi humfungulia njia mtoaji,

nayo humleta mbele ya wakuu.

17 Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi,

hadi mwingine ajitokezapo na kumwuliza maswali.

18 Kupiga kura hukomesha mashindano

na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.

19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika

kuliko mji uliozungushiwa ngome,

nayo mabishano ni kama malango

ya ngome yenye makomeo.

20 Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake,

atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.

21 Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi,

nao waupendao watakula matunda yake.

22 Apataye mke apata kitu chema

naye ajipatia kibali kwaBwana.

23 Mtu maskini huomba kuhurumiwa

bali tajiri hujibu kwa ukali.

24 Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu,

bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/18-d3e050454d824e01ec02c50d2a6a2997.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fifteen + 10 =