Mithali 2

Faida Za Hekima

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

2 kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

3 na kama ukiita busara

na kuita kwa sauti ufahamu,

4 na kama utaitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

5 ndipo utakapoelewa kumchaBwana

na kupata maarifa ya Mungu.

6 Kwa maanaBwanahutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

7 Huifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,

yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,

8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki

na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki

na sawa, katika kila njia nzuri.

10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,

nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

11 Busara itakuhifadhi

na ufahamu utakulinda.

12 Hekima itakuokoa kutoka katika njia za waovu,

kutoka watu ambao maneno yao yamepotoka,

13 wale waachao mapito yaliyonyooka

wakatembea katika njia za giza,

14 wale wapendao kutenda mabaya

na kufurahia upotovu wa ubaya,

15 ambao mapito yao yamepotoka

na ambao ni wapotovu katika njia zao.

16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,

kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno

ya kushawishi kutenda ubaya,

17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake

na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo

na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

19 Hakuna ye yote aendaye kwake akarudi,

au kufikia mapito ya uzima.

20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema

na kushikamana na mapito ya wenye haki.

21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,

nao wasio na lawama watabakia ndani yake,

22 bali waovu watakatiliwa mbali kutoka katika nchi,

nao wasio waaminifu watang’olewa kutoka humo.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/2-ea08cd3b924427c425c645de0f3f04e9.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five × 4 =