Mithali 3

Faida Nyingine Za Hekima

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu,

bali zitunze amri zangu moyoni mwako,

2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako

na kukuletea mafanikio.

3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;

vifunge shingoni mwako,

viandike katika ubao wa moyo wako.

4 Ndipo utapata kibali na jina zuri

mbele za Mungu na mwanadamu.

5 MtumainiBwanakwa moyo wako wote

wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

6 katika njia zako zote mkiri yeye,

naye atayanyosha mapito yako.

7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe,

mcheBwanaukajiepushe na uovu.

8 Hii itakuletea afya mwilini mwako,

na mafuta kwenye mifupa yako.

9 MheshimuBwanakwa mali zako na

kwa malimbuko ya mazao yako yote;

10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika,

viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

11 Mwanangu, usidharau marudi yaBwana

na usichukie kukaripiwa naye,

12 kwa sababuBwanahuwarudi wale awapendao,

kama vile baba afanyavyo

kwa mwana apendezwaye naye.

13 Heri mtu yule aonaye hekima,

mtu yule apataye ufahamu,

14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha

na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.

15 Hekima ana thamani kuliko marijani,

hakuna cho chote unachokitamani

kinachoweza kulinganishwa naye.

16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume,

katika mkono wake wa kushoto

kuna utajiri na heshima.

17 Njia zake zinapendeza,

mapito yake yote ni amani.

18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;

wale wamshikao watabarikiwa.

19 Kwa hekimaBwanaaliiweka misingi ya dunia,

kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;

20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,

nayo mawingu yanadondosha umande.

21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,

usiache vitoke machoni pako;

22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako

na pambo la neema shingoni mwako.

23 Kisha utaenda katika njia yako salama,

wala mguu wako hautajikwaa;

24 ulalapo, hautaogopa;

ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.

25 Usiogope maafa ya ghafula

au maangamizi yanayowapata waovu,

26 kwa kuwaBwanaatakuwa tumaini lako

na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.

27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili

ikiwa katika uwezo wako kutenda.

28 Usimwambie jirani yako,

“Njoo baadaye, nitakupa kesho,”

wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.

29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,

ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.

30 Usimshtaki mtu bila sababu,

wakati hajakutenda dhara lo lote.

31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri

wala kuchagua njia yake iwayo yote,

32 kwa kuwaBwanahumchukia mtu mpotovu,

lakini siri yake iko kwa mwenye haki.

33 Laana yaBwanai juu ya nyumba ya mwovu,

lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.

34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki kwa kiburi

lakini huwapa neema wanyenyekevu.

35 Wenye hekima hurithi heshima,

bali huwaaibisha wapumbavu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/3-0d7d31ecef474efe5f9e52c71d027fe1.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fourteen − 7 =