Mithali 21

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono waBwana;

huuongoza kama mkondo wa maji, po pote apendapo.

2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,

baliBwanahuupima moyo.

3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika

zaidi kwaBwanakuliko dhabihu.

4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,

ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!

5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,

kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.

6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo

ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.

7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,

kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.

8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,

bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.

9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba

kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya,

jirani yake hapati huruma kutoka kwake.

11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,

mjinga hupata hekima;

wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,

hupata maarifa.

12 Mwenye haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,

naye atawaangamiza waovu.

13 Kama mtu akizibia masikio kilio cha maskini,

yeye pia atalia wala hatajibiwa.

14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira

na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.

15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,

bali kitisho kwa watenda mabaya.

16 Mtu anayepotea kutoka katika mapito ya ufahamu,

hupumzika katika kundi la waliokufa.

17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,

ye yote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.

18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,

nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.

19 Ni afadhali kuishi jangwani

kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.

20 Katika nyumba ya mwenye hekima

kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,

lakini mtu mpumbavu

hutafuna vyote alivyo navyo.

21 Yeye afuatiaye haki na upendo

hupata uzima, mafanikio na heshima.

22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,

na kuangusha ngome wanazozitegemea.

23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake

hujilinda na maafa.

24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;

hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.

25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,

kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.

26 Mchana kutwa hutamani zaidi,

lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.

27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,

si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

28 Shahidi wa uongo ataangamia,

bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.

29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,

bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.

30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango

unaoweza kufaulu dhidi yaBwana.

31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,

bali ushindi huwa kwaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/21-5fdc06d6f9d93f0c2ebc3a7a2601e682.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

15 − four =