Mithali 22

1 Heri kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi,

kuheshimiwa ni bora kuliko fedha au dhahabu.

2 Tajiri na maskini wanafanana kwa hili:

Bwanani Muumba wao wote.

3 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha,

bali mjinga huendelea mbele kama kipofu nayo ikamtesa.

4 Unyenyekevu na kumchaBwana

huleta utajiri, heshima na uzima.

5 Katika mapito ya waovu kuna miiba na mitego,

bali yeye ailindaye nafsi yake hukaa mbali nayo.

6 Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea,

naye hataiacha hata akiwa mzee.

7 Matajiri huwatawala maskini

naye akopaye ni mtumwa wa akopeshaye.

8 Yeye aupandaye uovu huvuna taabu,

nayo fimbo ya ghadhabu yake itaangamizwa.

9 Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa

kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.

10 Mfukuze mwenye dhihaka,

nayo mashindano yatatoweka;

ugomvi na matukano vitakoma.

11 Yeye apendaye moyo safi na yeye ambaye maneno yake ni ya neema,

mfalme atakuwa rafiki yake.

12 Macho yaBwanahulinda maarifa,

bali huyapinga maneno ya asiye mwaminifu.

13 Mvivu husema, “Kuna simba nje!”

au, “Nitauawa huko njiani!”

14 Kinywa cha mwanamke kahaba ni shimo refu;

yeye aliye chini ya ghadhabu yaBwana

atatumbukia ndani yake.

15 Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto,

bali fimbo ya adhabu itaufukuzilia mbali naye.

16 Yeye amuoneaye maskini ili kujiongezea mali,

naye ampaye tajiri zawadi, wote huwa maskini.

Misemo Ya Wenye Hekima

17 Tega sikio na usikie misemo ya wenye hekima,

elekeza moyo wako kwenye yale nifundishayo,

18 kwa maana inapendeza unapoyahifadhi moyoni mwako

na kuwa nayo yote tayari midomoni mwako.

19 Ili tumaini lako liwe katikaBwana,

hata wewe, ninakufundisha leo.

20 Je, sijakuandikia misemo thelathini,

misemo ya mashauri na maarifa,

21 kukufundisha maneno ya kweli na ya kuaminika,

ili uweze kutoa majibu sahihi

kwake yeye aliyekutuma?

22 Usiwadhulumu maskini kwa hila kwa sababu ni maskini,

wala kumdhulumu mhitaji mahakamani,

23 kwa sababuBwanaatalichukua shauri lao

naye atawateka wao waliowateka.

24 Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka,

usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,

25 la sivyo utajifunza njia zake

na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.

26 Usiwe mwenye kupana mikono katika rehani,

au kuweka dhamana kwa ajili ya madeni.

27 Kama ukikosa njia ya kulipa,

kitanda chako ukilaliacho

kitachukuliwa ukiwa umekilalia.

28 Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani

lililowekwa na baba zako.

29 Je, unamwona mtu stadi katika kazi yake?

Atahudumu mbele ya wafalme;

hatahudumu mbele ya watu duni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PRO/22-921199a38e30e30f2a58a145b3c75beb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

seventeen − 11 =