Nehemiah 7

1 Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na kuweka milango, waliteuliwa mabawabu wa lango, waimbaji na Walawi.

2 Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.

3 Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Wakati walinzi wa malango wakiwa kwenye zamu, wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”

Orodha Ya Waliorudi Toka Uhamishoni

4 Mji ulikuwa mkubwa tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.

5 Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi iliyoandikwa ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:

6 Hawa ndio watu wa jimbo waliorudi kutoka utumwani uhamishoni walikokuwa wamepelekwa na Mfalme Nebukadneza wa Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,

7 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana):

Orodha ya watu wa Israeli:

8 wazao wa Paroshi 2,172
9 wazao wa Shefatia 372
10 wazao wa Ara 652
11 wazao wa Pahath-Moabu (kupitia ukoo wa Yeshua na Yoabu) 2,818
12 wazao wa Elamu 1,254
13 wazao wa Zatu 845
14 wazao wa Zakai 760
15 wazao wa Binui 648
16 wazao wa Bebai 628
17 wazao wa Azgadi 2,322
18 wazao wa Adonikamu 667
19 wazao wa Bigwai 2,067
20 wazao wa Adini 655
21 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 wazao wa Hashumu 328
23 wazao wa Besai 324
24 wazao wa Harifu 112
25 wazao wa Gibeoni 95
26 watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 watu wa Anathothi 128
28 watu wa Beth-Azmawethi 42
29 watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 watu wa Rama na Geba 621
31 watu wa Mikmashi 122
32 watu wa Betheli na Ai 123
33 watu wa Nebo 52
34 watu wa Elamu 1,254
35 watu wa Harimu 320
36 watu wa Yeriko 345
37 watu wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 watu wa Senaa 3,930

39 Makuhani:

wazao wa Yedaya (kupitia familia ya Yeshua) 973
40 wazao wa Imeri 1,052
41 wazao wa Pashuri 1,247
42 wazao wa Harimu 1,017

43 Walawi:

wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia ukoo wa Hodavia) 74

44 Waimbaji:

wazao wa Asafu 148

45 Mabawabu wa malango:

wazao waShalumu, Ateri, Talmoni,Akubu, Hatita na Shobai 138

46 Wanethiniwa Hekaluni:

wazao wa

Siha, Hasufa, Tabaothi,

47 Kerosi, Sia, Padoni,

48 Lebana, Hagaba, Shalmai,

49 Hanani, Gideli, Gahari,

50 Reaya, Resini, Nekoda,

51 Gazamu, Uza, Pasea,

52 Besai, Meunimu, Nefusimu,

53 Bakbuki, Hakufa, Harhuri,

54 Basluthi, Mehida, Harsha,

55 Barkosi, Sisera, Tema,

56 Nesia na Hatifa.

57 Wazao wa watumishi wa Solomoni:

wazao wa

Sotai, Soferethi, Perida,

58 Yaala, Darkoni, Gideli,

59 Shefatia, Hatili,

Pokereth-Hazebaimu na Amoni.

60 Wanethini wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392

61 Wafuatao ni watu waliorudi kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamii zao zilitokana na Israeli:

62 wazao waDelaya, Tobia na Nekoda 642

63 Na kutoka miongoni mwa makuhani:

wazao wa

Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo.)

64 Hawa walitafuta katika orodha ya jamii zao, lakini hawakuonekana kwa hiyo waliondolewa katika ukuhani kama watu najisi.

65 Kwa hiyo, Tirshathaaliagiza kuwa wasile cho chote miongoni mwa vyakula vitakatifu mpaka atakapopatikana kuhani ahudumuye kwa Urimu na Thumimu.

66 Jumla ya watu wote waliorudi kutoka utumwani uhamishoni walikuwa 42,360;

67 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwemo waimbaji wanaume na wanawake 245.

68 Walikuwako farasi 736, nyumbu 245

69 ngamia 435 na punda 6,720.

70 Baadhi ya wakuu wa mbari walichangia kazi ya ujenzi. Tirshatha alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000za dhahabu, mabakuli 50 na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.

71 Baadhi ya wakuu wa mbari walikabidhi kwenye hazina kwa ajili ya kazi darkoni 20,000 za dhahabuna mane 2,200za fedha.

72 Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha na mavazi sitini na saba ya makuhani.

73 Makuhani, Walawi, mabawabu wa malango, waimbaji na Wanethini, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli wengine wote, waliishi katika miji yao wenyewe.

Ezara Asoma Sheria

Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NEH/7-4584123c74f1e3ac9b4d583f95216276.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine + eleven =