Sefania 1

1 Neno laBwanaambalo lilimjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:

Onyo La Maangamizi Yanayokuja

2 Bwanaasema,

“Nitafagia kila kitu

kutoka kwenye uso wa dunia.”

3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama;

nitafagilia mbali ndege wa angani

na samaki wa baharini.

Wafanyao maovu wajikwae, pamoja na hao waovu,

nami nitamkatilia mbali mwanadamu

atoke katika dunia,”

asemaBwana.

Dhidi Ya Yuda

4 “Nitaiadhibu Yuda

na wote wakaao Yerusalemu.

Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali

kila mabaki ya Baali,

majina ya wapagani na makuhani

waabuduo sanamu:

5 wale ambao husujudu juu ya mapaa

kuabudu jeshi la vitu vya angani,

wale ambao husujudu na kuapa kwaBwana

na ambao pia huapa kwa Malkamu,

6 wale ambao wanaacha kumfuataBwana,

wala hawamtafutiBwana

wala kutaka shauri lake.

7 Nyamazeni mbele zaBwanaMwenyezi,

kwa maana siku yaBwanaiko karibu.

Bwanaameandaa dhabihu,

amewaweka wakfu wale aliowaalika.

8 Katika siku ya dhabihu yaBwana

nitawaadhibu wakuu

na wana wa mfalme

na wale wote wanaovaa

nguo za kigeni.

9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao

hukwepa kukanyaga kizingiti,

ambao hujaza hekalu la miungu yao

kwa jeuri na udanganyifu.”

10 Bwanaasema, “Katika siku hiyo

kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki,

maombolezo kutoka mtaa wa pili,

na mshindo mkubwa kutoka vilimani.

11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni;

wafanyabiashara wenu

wote wameangamizwa,

wote ambao wanafanya

biashara ya fedha

wameangamizwa.

12 Wakati huo nitasaka katika mji wa Yerusalemu kwa taa

na kuwaadhibu wale ambao

wanakaa katika hali ya kuridhika,

ambao ni kama divai

iliyobaki kwenye machicha,

ambao hudhani, ‘Bwanahatafanya lo lote,

jema au baya.’

13 Utajiri wao utatekwa nyara,

nyumba zao zitabomolewa.

Watajenga nyumba,

lakini hawataishi ndani yake;

watapanda mizabibu

lakini hawatakunywa divai yake.

Siku Kubwa Ya Bwana

14 “Siku kubwa yaBwanaiko karibu:

iko karibu na inakuja haraka.

Sikilizeni! Kilio katika siku yaBwana

kitakuwa kichungu,

hata shujaa atapiga kelele.

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu,

siku ya fadhaa na dhiki,

siku ya uharibifu na ukiwa,

siku ya giza na utusitusi,

siku ya mawingu na giza nene,

16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita

dhidi ya miji yenye ngome

na dhidi ya minara mirefu.

17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea

kama wasio na macho,

kwa sababu wametenda dhambi

dhidi yaBwana.

Damu yao itamwagwa kama vumbi

na matumbo yao kama taka.

18 Fedha yao wala dhahabu yao

haitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya ghadhabu yaBwana.

Katika moto wa wivu wake

dunia yote itateketezwa,

kwa maana ataleta mwisho

wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/1-7b0933800ffffe34ebb9fa5dcbd54cdb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fourteen − 9 =