Sefania 2

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja,

enyi taifa lisilo na aibu,

2 kabla ya wakati ulioamuriwa haujafika

na siku ile inayopeperusha kama makapi,

kabla hasira kali yaBwanahaijaja juu yenu,

kabla siku ya ghadhabu yaBwana

haijaja juu yenu.

3 MtafuteniBwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi,

ninyi ambao hufanya lile analoamuru.

Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu;

labda mtahifadhiwa

siku ya hasira yaBwana.

Dhidi Ya Ufilisti

4 Gaza utaachwa

na Ashkeloni utaachwa magofu.

Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu

na Ekroni utang’olewa.

5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari,

Enyi Wakerethi;

neno laBwanaliko dhidi yenu,

Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti.

“Mimi nitawaangamiza,

wala hakuna atakayebaki.”

6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi,

patakuwa mahali pa wachungaji

na mazizi ya kondoo.

7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda,

hapo watapata malisho.

Wakati wa jioni watajilaza chini

katika nyumba za Ashkeloni.

BwanaMungu wao atawatunza,

naye atawarudishia wafungwa wao.

Dhidi Ya Moabu Na Amoni

8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu

nazo dhihaka za Waamoni,

ambao waliwatukana watu wangu

na kufanya vitisho dhidi ya nchi yao.

9 Hakika, kama niishivyo,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mungu wa Israeli,

“hakika Moabu itakuwa kama Sodoma,

Waamori kama Wagomora:

mahali pa magugu na mashimo ya chumvi,

nchi ya ukiwa milele.

Mabaki ya watu wangu watawateka nyara;

mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”

10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao,

kwa kutukana na kudhihaki

watu waBwanaMwenye Nguvu Zote.

11 Bwanaatakuwa wa kutisha kwao

wakati atakapoangamiza

miungu yote ya nchi.

Mataifa katika kila pwani yatamwabudu,

kila moja katika nchi yake.

Dhidi Ya Kushi

12 “Ninyi pia, Ee Wakushi,

mtauawa kwa upanga wangu.”

Dhidi Ya Ashuru

13 Mungu atanyosha mkono wake dhidi ya kaskazini

na kuangamiza Waashuru,

akiiacha Ninawi ukiwa

na pakame kama jangwa.

14 Makundi ya kondoo na ng’ombe yatajilaza pale,

viumbe vya kila aina.

Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba

wataishi juu ya nguzo zake.

Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani,

kifusi kitakuwa milangoni,

boriti za mierezi zitaachwa wazi.

15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha

wakijisikia salama.

Ulisema moyoni mwako,

“Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.”

Jinsi gani umekuwa gofu,

mahali pa kulala wanyama pori!

Wote wanaopita kando yake wanauzomea

na kutikisa mkono kwa dharau.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/2-1b18ca38d2ccf242c0429323ed47e58d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

one × 5 =