Waamuzi 2

Malaika Wa Bwana Huko Bokimu

1 Malaika waBwanaakakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.

2 Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu zao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?

3 Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”

4 Malaika waBwanaalipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.

5 Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtoleaBwanasadaka.

Kifo Cha Yoshua

6 Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.

7 Watu wakamtumikiaBwanasiku zote za maisha za Yoshua na za wazee walioishi kuliko Yoshua, ambao walikuwa wameona mambo makuu ambayoBwanaalikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.

8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi waBwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.

9 Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresikatika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.

10 Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjuaBwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.

11 Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni paBwanana kuwatumikia Mabaali.

12 WakamwachaBwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. WakamkasirishaBwana,

13 kwa sababu walimwacha yeye na kutumikia Baali na Maashtorethi.

14 Hivyo hasira yaBwanaikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.

15 Po pote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono waBwanaulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.

16 NdipoBwanaakawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.

17 Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri zaBwana.

18 Kila maraBwanaalipowainulia mwamuzi,Bwanaalikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwaBwanaaliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.

19 Lakini kila mara mwamuzi alipokufa, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.

20 Kwa hiyoBwanaakawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,

21 mimi nami sitafukuza taifa lo lote ambalo Yoshua aliliacha alipokufa.

22 Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia yaBwanana kuenenda katika hiyo kama baba zao walivyofanya.”

23 Bwanaalikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JDG/2-2c8fb430d3a9cedf1d755d1cac3f4efe.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

three × 1 =