Waamuzi 3

Mataifa Yaliyobaki Katika Ile Nchi

1 Haya ndiyo mataifaBwanaaliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita yo yote ya Kanaani

2 (alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali):

3 wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi.

4 Waliachwa ili kuwajaribu Waisraeli kuona kama wangetii amri zaBwana, alizokuwa amewapa baba zao kwa mkono wa Mose.

5 Waisraeli wakaishi miongoni mwa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

6 Wakawaoa binti zao, nao wakawatoa binti zao waolewe na wana wa hayo mataifa, na kuitumikia miungu yao.

Othnieli

7 Waisraeli wakafanya maovu machoni paBwana, wakamsahauBwanaMungu wao na kutumikia Mabaali na Maashera.

8 Hasira yaBwanaikawaka dhidi ya Israeli, hivyo akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu-Naharaimuambaye Israeli walikuwa chini yake wakimtumikia kwa muda wa miaka minane.

9 WalipomliliaBwana, yeye akawainulia mwokozi, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, ambaye aliwaokoa.

10 Roho waBwanaakaja juu yake, hivyo akawa mwamuzi wa Israeli, akaenda vitani.Bwanaakamtia Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu mikononi mwa Othnieli, naye akamshinda.

11 Hivyo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arobaini, mpaka Othnieli mwana wa Kenazi alipokufa.

Ehudi

12 Waisraeli wakafanya yaliyo maovu mbele zaBwanatena, kwa kuwa walifanya maovu hayoBwanaakamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli.

13 Egloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende.

14 Waisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.

15 Waisraeli wakamlilia tenaBwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi.

16 Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye makali kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja, akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume.

17 Akamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana.

18 Baada ya Ehudi kumkabidhi ule ushuru, wale watu waliokuwa wameubeba huo ushuru aliwaruhusu waende zao.

19 Yeye mwenyewe akafuatana nao hadi kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe karibu na Gilgali, ndipo yeye akarudi, akafika kwa Egloni na kusema, “Ee Mfalme, ninao ujumbe wa siri kwa ajili yako.”

Mfalme akasema, “Nyamazeni kimya!” Nao wale waliomhudumia wote wakamwacha, wakatoka nje.

20 Ndipo Ehudi akamsogelea alipokuwa ameketi peke yake kwenye chumba cha juu cha jumba lake la kifalme la majira ya kiangazi, na kusema, “Ninao ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Mfalme alipokuwa anainuka kutoka kwenye kiti chake,

21 Ehudi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kuufuta ule upanga aliokuwa ameufunga kwenye paja lake la kulia na kuuchomeka tumboni mwa Mfalme Egloni kwa nguvu.

22 Hata mpini nao ukazama tumboni pamoja na upanga wenyewe, nao upanga ukatokea mgongoni mwake. Ehudi hakuuchomoa huo upanga, nayo mafuta yakashikamana juu ya panga.

23 Ehudi akatoka nje barazani; akamfungia milango ya chumba cha juu na kuifunga kwa funguo.

24 Baada ya kuondoka, watumishi wakaja na kukuta milango ya chumba cha juu imefungwa kwa funguo. Wakasema, “Bila shaka amejipumzisha kwenye chumba cha ndani cha nyumba yake ya majira ya kiangazi.”

25 Wakangoja hata wakawa na fadhaa, basi alipokuwa hakufungua milango ya chumba, wakachukua funguo na kuifungua. Tazama wakaona bwana wao amelala sakafuni, amekufa.

26 Walipokuwa wangali wanangoja, Ehudi akatoroka, akapita hapo kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe na kukimbilia Seira.

27 Alipofika huko, akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakatelemka pamoja naye kutoka vilimani, yeye akiwa anawaongoza.

28 Akawaagiza, “Nifuateni, kwa kuwaBwanaamewatia Moabu, adui zenu, mikononi mwenu.” Kwa hiyo wakatelemka wakamfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kuelekea Moabu, wala hawakuacha mtu ye yote kuvuka.

29 Wakati huo wakawaua Wamoabu watu waume wapatao 10,000 ambao wote walikuwa wenye nguvu na mashujaa; hakuna mtu ye yote aliyetoroka.

30 Siku ile Moabu wakashindwa na Israeli, nayo nchi ikawa na amani kwa miaka themanini.

Shamgari

31 Baada ya Ehudi akaja Shamgari mwana wa Anathi, aliyewapiga Wafilisti 600 kwa fimbo iliyochongoka ya kuongozea ng’ombe. Naye pia akawaokoa Waisraeli.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JDG/3-c18a0782f94d8effb4cc5ff79b00e745.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nineteen − fifteen =