Waamuzi 5

Wimbo Wa Debora

1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:

2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza,

wakati watu wanapojitoa

kwa hiari yao wenyewe:

mhimidiniBwana!

3 “Sikieni hili, enyi wafalme!

Sikilizeni, enyi watawala!

NitamwimbiaBwana, nitaimba;

kwa wimbo nitamhimidiBwana,

Mungu wa Israeli.

4 “EeBwana, ulipotoka katika Seiri,

ulipopita katika mashamba ya Edomu,

nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga,

naam, mawingu yakamwaga maji.

5 Milima ilitetemeka mbele zaBwana,

hata ule wa Sinai,

mbele zaBwana,

Mungu wa Israeli.

6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi,

katika siku za Yaeli,

barabara kuu hazikuwa na watu;

wasafiri walipita njia za kando.

7 Mashujaa walikoma katika Israeli,

walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka,

nilipoinuka kama mama katika Israeli.

8 Walipochagua miungu migeni,

vita vilikuja katika malango ya mji,

hapakuonekana ngao wala mkuki

miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.

9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli,

pamoja na wale wanaojitoa wenyewe

kwa hiari yao miongoni mwa watu.

MhimidiniBwana!

10 “Nanyi mpandao punda weupe,

mkiketi juu ya matandiko ya thamani,

nanyi mtembeao barabarani,

fikirini

11 juu ya sauti za waimbaji

mahali pa kunyweshea maji.

Wanasimulia matendo ya haki yaBwana,

matendo ya haki ya mashujaa wake

katika Israeli.

“Ndipo watu waBwana

walipotelemka malangoni pa mji.

12 ‘Amka, amka! Debora!

Amka, amka, uimbe!

Ee Baraka! Inuka,

chukua mateka wako uliowateka,

Ee mwana wa Abinoamu.’

13 “Ndipo mabaki ya watu

wakashuka dhidi ya wenye nguvu,

watu waBwana,

wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.

14 Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki;

Benyamini akiwa miongoni

mwa watu waliokufuata.

Kutoka Makiri wakashuka viongozi,

na kutoka Zabuloni wale washikao

fimbo ya jemadari.

15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora;

naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka,

wakija nyuma yake kwa mbio

wakielekea bondeni.

Katika jamaa za Reubeni,

palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.

16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo

kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi?

Katika jamaa za Reubeni,

palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.

17 Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani.

Naye Dani, kwa nini alikaa

kwenye merikebu siku nyingi?

Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari,

akikaa kwenye ghuba zake ndogo.

18 Watu wa Zabuloni walihatirisha maisha yao,

vile vile nao watu wa Naftali.

19 “Wafalme walikuja na kufanya vita;

wafalme wa Kanaani walipigana

huko Taanaki karibu na maji ya Megido,

lakini hawakuchukua fedha wala nyara.

20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana,

nyota kutoka katika njia zake

zilipigana na Sisera.

21 Mto wa Kishoni uliwasomba,

ule mto wa zamani, mto wa Kishoni.

Songa mbele, Ee nafsi yangu,

kwa ujasiri!

22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo:

farasi wake wenye nguvu

huenda mbio kwa kurukaruka.

23 Malaika waBwanaakasema, ‘Merozi alaaniwe.

Walaaniwe watu wake kwa uchungu,

kwa kuwa hawakuja kumsaidiaBwana,

kumsaidiaBwanadhidi ya hao wenye nguvu.’

24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote,

mkewe Heberi, Mkeni,

abarikiwe kuliko wanawake wote

waishio kwenye mahema.

25 Aliomba maji, naye akampa maziwa;

kwenye bakuli la heshima

akamletea maziwa mgando.

26 Akanyoosha mkono wake

akashika kigingi cha hema,

mkono wake wa kuume

ukashika nyundo ya fundi.

Akampiga Sisera kwa nyundo,

akamponda kichwa chake,

akamvunjavunja na kumtoboa

paji lake la uso.

27 Aliinama miguuni pa Yaeli,

akaanguka; akalala hapo.

Pale alipoinama miguuni pake,

alianguka;

pale alipoinamia, ndipo alipoanguka,

akiwa amekufa.

28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia;

nyuma ya dirisha alilia, akasema,

‘Mbona gari lake linachelewa kufika?

Mbona vishindo vya magari yake

vimechelewa?’

29 Wanawake wenye busara

kuliko wengine wote wakamjibu;

naam, husema moyoni mwake,

30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara:

msichana mmoja au wawili kwa kila mtu,

mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara,

mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa,

mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu:

yote haya kuwa nyara?’

31 “Adui zako wote na waangamie, EeBwana!

Bali wote wakupendao na wawe kama jua

lichomozavyo kwa nguvu zake.”

Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JDG/5-54532687ea068db9b0f4449cc384bb0a.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

one × five =