Yeremia 11

Agano Limevunjwa

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwaBwana:

2 “Sikia maneno ya Agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio katika Yerusalemu.

3 Waambie kwamba hili ndilo asemaloBwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu yule ambaye hatayatii maneno ya Agano hili,

4 yaani maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.

5 Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.”

Nikajibu, “Amen,Bwana.”

6 Bwanaakaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya Agano hili na kuyafuata.

7 Tangu wakati ule nilipowapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”

8 Lakini hawakusikiliza wala kujali, badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za Agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata lakini wao hawakulishika.’ ”

9 KishaBwanaakaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi katika Yerusalemu.

10 Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja Agano nililofanya na baba zao.

11 Kwa hivyo, hili ndilo asemaloBwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia mimi sitawasikiliza.

12 Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.

13 Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, Ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’

14 “Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yo yote au usinisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.

15 “Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu

anapofanya mashauri yake maovu na wengi?

Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza

kuondolea mbali adhabu yako?

Unapojiingiza katika ubaya wako,

ndipo unashangilia.”

16 Bwanaalikuita mti wa mzeituni uliostawi

ulio na matunda mazuri kwa sura.

Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu

atautia moto,

nayo matawi yake yatavunjika.

17 BwanaMwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.

Shauri Baya Dhidi Ya Yeremia

18 Kwa sababuBwanaalinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.

19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni, mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema,

“Sisi na tuuangamize mti na matunda yake;

nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai,

ili kwamba jina lake lisikumbukwe tena.”

20 Lakini, EeBwanaMwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki,

nawe uchunguzaye moyo na akili,

mimi na nione ukiwalipiza wao kisasi,

kwa maana kwako nimeweka shauri langu.

21 “Kwa hiyo hili ndiloBwanaasemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina laBwanala sivyo utakufa kwa mikono yetu’:

22 kwa hiyo hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.

23 Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/11-b3ebb764a2340f0f013ad7dfbf8fa44a.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

one + seven =