Yeremia 15

Adhabu Isiyoepukika

1 KishaBwanaakaniambia: “Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele zangu, moyo wangu usingewaelekea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende!

2 Nao kama wakikuuliza, ‘Tuende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndiloBwanaasemalo:

“ ‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe;

waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga;

waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa:

waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’ ”

3 Bwanaasema, “Nitatuma aina nne ya waharabu dhidi yao, upanga ili kuua na mbwa ili wakokote mbali, ndege wa angani na wanyama wa nchi ili kula na kuangamiza.

4 Nitawafanya wawe machukizo kwa falme zote za dunia kwa sababu ya kile alichofanya Manase mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda huko Yerusalemu.

5 “Ni nani atakayekuhurumia, Ee Yerusalemu?

Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako?

Ni nani atakayesimama ili kuuliza

kuhusu hali yako?

6 Umenikataa mimi,” asemaBwana.

“Unazidi kukengeuka.

Hivyo nitanyosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza,

siwezi kuendelea kukuonea huruma.

7 Nitawapepeta kwa uma wa kupepetea

kwenye malango ya miji katika nchi.

Nitaleta msiba na maangamizi juu ya watu wangu,

kwa maana hawajabadili njia zao.

8 Nitawafanya wajane wao kuwa wengi

kuliko mchanga wa bahari.

Wakati wa adhuhuri nitamleta mharabu

dhidi ya mama wa vijana wao waume;

kwa ghafula nitaleta juu yao

maumivu makuu na hofu kuu.

9 Mama mwenye watoto saba atazimia

na kupumua pumzi yake ya mwisho.

Jua lake litatua kungali bado mchana,

atatahayarika na kufedheheka.

Wale wote waliobaki nitawaua kwa upanga

mbele ya adui zao,”

asemaBwana.

10 Ole wangu, mama yangu, kwamba ulinizaa,

mtu ambaye ulimwengu wote

unashindana na kugombana naye!

Sikukopa wala sikukopesha,

lakini kila mmoja ananilaani.

11 Bwanaakasema,

“Hakika nitakuokoa kwa kusudi jema,

hakika nitawafanya adui zako wakuombe msaada

nyakati za maafa na nyakati za dhiki.

12 “Je, mtu aweza kuvunja chuma,

chuma kitokacho kaskazini na shaba?

13 Utajiri wako na hazina zako nitavitoa kuwa nyara,

bila gharama,

kwa sababu ya dhambi zako zote

katika nchi yako yote.

14 Nitakufanya uwe mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa katika hasira yangu moto umewashwa

utakaowaka juu yako daima.”

15 Wewe unajua, EeBwana,

unikumbuke na unitunze mimi.

Lipiza kisasi juu ya watesi wangu.

Kwa uvumilivu wako usiniondolee mbali;

kumbuka jinsi ninavyoshutumiwa.

16 Maneno yako yalipokuja, niliyala;

yakawa shangwe yangu

na furaha ya moyo wangu,

kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako,

EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote.

17 Kamwe sikuketi katika kundi la wafanyao sherehe,

wala kamwe sikujifurahisha pamoja nao;

niliketi peke yangu kwa sababu mkono wako

ulikuwa juu yangu

na wewe ulikuwa umenijaza hasira.

18 Kwa nini maumivu yangu hayakomi

na jeraha langu ni la kuhuzunisha

wala haliponyeki?

Je, utakuwa kwangu kama kijito cha udanganyifu,

kama chemchemi iliyokauka?

19 Kwa hiyo hili ndilo asemaloBwana:

“Kama ukitubu, nitakurejeza

ili uweze kunitumikia;

kama ukinena maneno yenye maana,

wala si ya upuzi,

utakuwa mnenaji wangu.

Watu hawa ndio watakaokugeukia,

wala si wewe utakayewageukia wao.

20 Nitakufanya wewe uwe ukuta kwa watu hawa,

ngome ya ukuta wa shaba;

watapigana nawe

lakini hawatakushinda,

kwa maana mimi niko pamoja nawe

kukuponya na kukuokoa,”

asemaBwana.

21 “Nitakuokoa kutoka katika mikono ya waovu,

na kukukomboa kutoka katika makucha ya watu wakatili.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/15-4548a78186f4e02936d325653f06a3bb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eighteen + eighteen =