Yeremia 2

Israeli Amwacha Mungu

1 Neno laBwanalilinijia kusema,

2 “Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu:

“ ‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako,

jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi

na kunifuata katika jangwa lile lote,

katika nchi isiyopandwa mbegu.

3 Israeli alikuwa mtakatifu kwaBwana,

malimbuko ya kwanza ya mavuno yake;

wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia,

nayo maafa yaliwakumba,’ ”

asemaBwana.

4 Sikia neno laBwana, Ee nyumba ya Yakobo,

nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.

5 Hivi ndivyo asemavyoBwana:

“Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu,

hata wakatangatanga mbali nami hivyo?

Walifuata sanamu zisizofaa,

nao wenyewe wakawa hawafai.

6 Hawakuuliza, ‘Yuko wapiBwana,

aliyetupandisha kutoka Misri

na kutuongoza kupitia katika nyika kame,

kupitia katika nchi ya majangwa na mabonde,

nchi ya ukame na giza,

nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake

wala hakuna mtu aishiye humo?’

7 Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu

mpate kula matunda yake

na utajiri wa mazao yake.

Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu

na kuufanya urithi wangu chukizo.

8 Makuhani hawakuuliza,

‘Yuko wapiBwana?’

Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi;

viongozi waliasi dhidi yangu.

Manabii walitabiri kwa jina la Baali,

wakifuata sanamu zisizofaa.

9 “Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,”

asemaBwana.

“Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.

10 Vuka, nenda ng’ambo mpaka pwani ya Kitimunawe uangalie,

tuma watu waende Kedari na wachunguze kwa makini,

uone kama kumekuwapo kitu kama hiki.

11 Je, taifa limebadili miungu yake wakati wo wote?

(Hata ingawa hao si miungu kamwe.)

Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao

kwa sanamu zisizofaa kitu.

12 Shangaeni katika hili, Ee mbingu,

nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,”

asemaBwana.

13 “Watu wangu wametenda dhambi mbili:

Wameniacha mimi,

niliye chemchemi ya maji yaliyo hai,

nao wamejichimbia visima vyao wenyewe,

visima vilivyobomoka visivyoweza kuhifadhi maji.

14 Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa?

Kwa nini basi amekuwa mateka?

15 Simba wamenguruma;

wamemngurumia.

Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa;

miji yake imeteketezwa nayo imeachwa haina watu.

16 Pia watu wa Memfisina Tahpanhesi

wamevunja taji ya kichwa chako.

17 Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe

kwa kumwachaBwana, Mungu wako

alipowaongoza njiani?

18 Sasa kwa nini uende Misri

kunywa maji kutoka katika Shihori?

Nawe kwa nini kwenda Ashuru

kunywa maji yatokayo katika Mto Eufrati?

19 Uovu wako utakuadhibu;

kurudi nyuma kwako kutakukemea.

Basi kumbuka, utambue

jinsi lilivyo ovu na chungu kwako

unapomwachaBwanaMungu wako

na kutokuwa na hofu yangu,”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote.

20 “Zamani nilivunja nira yako

na kukatilia mbali vifungo vyako;

ukasema, ‘Sitakutumikia’!

Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu

na chini ya kila mti uliotanda matawi yake

ulijilaza kama kahaba.

21 Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana,

mkamilifu na wa mbegu nzuri.

Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami,

ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?

22 Hata ujisafishe kwa magadi

na kutumia sabuni nyingi,

bado doa la hatia yako liko mbele zangu,”

asemaBwanaMwenyezi.

23 “Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi,

sijawafuata Mabaali’?

Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni;

fikiri uliyoyafanya.

Wewe ni ngamia jike mwenye mbio

ukikimbia hapa na pale,

24 punda-mwitu aliyezoea jangwa,

anayenusa upepo, katika tamaa yake kubwa:

akiwa katika wakati wake wa kuhitaji mbegu

ni nani awezae kumzuia?

Madume yo yote yanayomfuatilia

hayana haja ya kujichosha;

wakati wa kupandwa kwake watampata tu.

25 Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu

na koo lako liwe limekauka.

Lakini ulisema, ‘Haina maana!

Ninaipenda miungu ya kigeni,

nami ni lazima niifuatie.’

26 “Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa,

hivyo ndivyo na nyumba ya Israeli inavyoaibishwa,

wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao,

makuhani wao na manabii wao.

27 Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’

tena wanaliambia jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’

Wamenipa visogo vyao

wala hawakunigeuzia nyuso zao;

lakini wakiwa katika taabu, wanasema,

‘Njoo utuokoe!’

28 Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea?

Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa

wakati mnapokuwa katika taabu!

Kwa maana mna miungu mingi

kama mlivyo na miji, Ee Yuda.

29 “Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu?

Ninyi nyote mmeniasi,”

asemaBwana.

30 “Ni bure tu nimeadhibu watu wako,

wala hukujirekebisha.

Upanga wako umewala manabii wako

kama simba mwenye njaa.

31 “Enyi wa kizazi hiki, kumbukeni neno laBwana:

“Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli

au nchi ya giza kuu?

Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura,

hatutarudi kwako tena’?

32 Je, mwanamwali husahau vitu vyake vilivyofanyizwa kwa vito,

bibi arusi husahau mapambo yake ya arusi?

Lakini watu wangu wamenisahau mimi,

tena kwa siku zisizo na hesabu.

33 Je, wewe ni fundi kiasi gani katika kufuatia mapenzi!

Hata wale wanawake wabaya kuliko wote

wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.

34 Katika nguo zako watu huona

damu ya uhai ya maskini wasio na hatia,

ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba.

Lakini pamoja na haya yote

35 unasema, ‘Sina hatia;

Mungu hajanikasirikia.’

Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema,

‘Mimi sijatenda dhambi.’

36 Kwa nini unatangatanga sana,

kubadili njia zako?

Utakatishwa tamaa na Misri

kama ulivyokatishwa na Ashuru.

37 Pia utaondoka mahali hapo

ukiwa umeweka mikono kichwani,

kwa kuwaBwanaamewakataa wale unaowatumainia;

hutasaidika kwa kupitia wao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/2-25231161dca39d00a279a7a85285a98f.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 + 15 =